Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Dennis Francis, Rais wa kikao cha 78 cha Baraza Kuu, akitoa muhtasari wa vipaumbele vyake kwa 2024. (Maktaba)
UN Photo/Eskinder Debebe

Rais wa Baraza Kuu: Umoja wa Mataifa sio tatizo

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Dennis Francis Pamoja na mambo mengine amesema Umoja wa Mataifa "sio tatizo" bali tatizo linatokana na kwamba baadhi ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanahisi wanaweza kukiuka mkataba wa Umoja wa Mataifa watakavyo na kukiuka sheria za kimataifa bila kuadhibiwa.

Timu ya Umoja wa Mataifa inajaribu kupeleka mafuta katika hospitali ya Nasser kupitia barabara zilizoharibiwa katikati ya Februari 2024.
© UNOCHA/Themba Linden

Taharuki yaongezeka Gaza huku msafara wa UN ukizuiliwa nje ya hospitali iliyoshambuliwa

Mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa yanayofanya kazi Ukanda wa Gaza uliokumbwa na vita yameonyesha kusikitishwa sana leo kutokana na kuendelea kwa vizuizi vya upatikanaji wa misaada ya kibinadamu vilivyowekewa na jeshi la Israel, baada ya magari ya kubebea wagonjwa yaliyokuwa yamewabeba wagonjwa kutoka hospitali iliyoshambuliwa mwishoni mwa juma kusimamishwa kwa saa kadhaa huku wahudumu wa afya wakisakwa na kuswekwa kizuizini.

Chakula kinasambazwa Omdurman, karibu na mji mkuu wa Sudan, Khartoum.
© Sudanese Red Crescent Society

Raia na wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu hawapaswi kushambuliwa - Clementine Nkweta-Salami

Nchini Sudan, Clementine Nkweta-Salami, ambaye ni naibu mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu na mratibu mkazi na misaada ya kibinadamu nchini Sudan, Clementine Nkweta-Salami, ameelezea kusikitishwa kwake na ripoti za mashambulizi dhidi ya wafanyakazi wa kujitolea wanaofanya kazi na mashirika ya kiraia, ikiwa ni pamoja na mipango inayoongozwa na jamii inayojulikana kama Vyumba vya Kukabiliana na Dharura, Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewaeleza leo Waandishi wa Habari jijini New York, Marekani.