Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Familia kutoka Eritrea ikiwa kwenye kituo cha muda Romani wakisubiriwa kuhamishwa hadi Netherlands.
© UNHCR/Stefan Lorint

Idadi ya wasaka hifadhi nchi ya tatu kuongezeka 2023

Zaidi ya wakimbizi milioni 2 mwaka ujao WA 2023 watahitaji kuhamishiwa nchi ya tatu ikiwa ni ongezeko kwa asilimia 36 ikilinganishwa na mahitaji ya mwaka huu ambayo ni wakimbizi milioni 1.5 pekee, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kupitia tathmini ya makadirio ya kuhamia nchi ya tatu kwa mwaka 2022.

Mji wa Bucha umeharibiwa vibaya kufuatia mashambulio Kyiv, mji mkuu wa Ukraine.
© WFP/Marco Frattini

Taarifa za awali zadokeza uhalifu wa kivita na ukiukwaji wa haki za binadamu Ukraine- Kamisheni 

Kamisheni iliyoundwa na Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu kuchunguza madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu na sheria za kimataifa za kibinadamu nchini Ukraine imetoa ripoti ya ziara yake ya kwanza nchini Ukraine na kusema ingawa haiko katika nafasi ya kuwa na vigezo vya kisheria au matokeo kamilifu, taarifa za awali zinadokeza kuweko kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na sheria za kimataifa za kiutu.