Mradi wa FAO wa dola milioni 17 kusaidia wakulima nchini Ukraine
Katika kushughulikia kupanda kwa bei za vyakula duniani kote shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limezindua mradi wa dola milioni 17 wa kusaidia wakulima nchini Ukraine ili kuokoa mavuno yao katika kipindi cha mwezi huu wa Julai na ujao wa Agosti huku wakihakikisha uuzaji wa mazao nje ya nchi.