Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno La Wiki

UN News Kiswahili

Neno la Wiki: Mkumbizi

Katika Neno la Wiki hii leo tunaangazia neno “Mkumbizi” na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania. 

Bwana Sigalla anasema neno hili lina maana zaidi ya moja, kwanza mtu anayesafisha mahali na kuondoa takataka, watu wengi wanamuita mfanyakazi lakini neno sahihi ni Mkumbizi.  Pili ni mtu afuataye wavunaji shambani na kuokota mavuno yaliyosalia kwa bahati na kutumia kama chakula chake.

Sauti
48"