Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno La Wiki

Neno la wiki: MEDE

Katika neno la wiki tunachambua neno "Mede", mchambuzi wetu leo ni Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa Maswala ya Mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.

Mede ina maana mbili, moja ni sehemu ya nyumba ambayo imetengwa kwa ajili ya kupumsikia,  yaani kupiga gumzi au kupumsikia na wageni maalumu kando na chumba cha kupumsikia na familia ya kwako. Pili, Mede ni mchezo wa watoto wa kujificha ili wenzake wamtafute, yaani wanaweza kujificha chini ya kitanda au sehemu nyingine ya siri.

Neno la wiki: FILA

Wiki hii tunaangazia neno "Fila" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Neno Fila ina maana mbili, ya kwanza neno hili hutumika katika msemo kwa maana ya "Ubaya" kwa mfano Lila na Fila haitangamani kumaanisha wema na ubaya havisikilizani, pili, Fila ni kifaa kinachotumiwa kujazia  wino kwenye mashine ya chapa.

Neno la Wiki- Mende

Katika neno la wiki Disemba 2 tunachambua neno Mende, mchambuzi wetu leo ni, Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.

Bwana Bakari anasema mende ni jamii ya mdudu ambaye amegawanyika kwa sehemu tatu, mende huyo anachukua majina tofauti kulingana na mazingira aliyomo, kombamwiko akiwa jikoni, akiwa kwenye sehemu chafu ni mende na akiwa ni wa kike amebeba mayai ni nyenze.