Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno La Wiki

Neno la wiki- Behewa

Wiki hii tunaangazia neno Behewe na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania. Buhewa lina zaidi ya maana moja, maana ya kwanza ni mahali pa wazi katika nyumba, maana nyingine ni sehemu au ghala ya kuwekea bidhaa kisawa chake ni bohari na nyingine ni sehemu ya gari moshi ya kuchukuliwa abiria au bidhaa.

Neno la wiki- Budi na Mujibu

Katika Neno la Wiki hii  Novemba 11 tunaangazia maneno budi na mujibu na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, huko nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema katika lugha ya kisawhili kuna maneno hayasimami peke yake na ni lazima yaanze na maneno mengine kwa mfano budi lazima lianze na kikanushi kama sina budi nalo mujibu lazima liambatane na ‘kwa’ yaani kwa mujibu wa

Neno la wiki- Mbulu

Katika neno la wiki tunachambua neno mbulu, mchambuzi wetu leo ni, Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa Maswala ya Mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA. Neno mbulu kama anayvofafanua Nuhu Bakari lina maana ya tabia za kiwenda wazimu.