Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

Photo: UNICEF Mozambique/Sergio Fernandez

Fanya kazi kwa bidhii utafanikiwa, acha kuwinda watu wenye ulemavu wa ngozi

Imani potofu kwa baadhi ya watu ya kwamba watatajirika iwapo watapeleka  viungo vya mtu mwenye ulemavu wa ngozi kwa waganga wa kienyeji imekuwa ikikatili maisha ya binadamu hao na kuwaacha wengine na madhara makubwa  ya kisaikolojia na kimwili katika maisha yao yote, wakati vitendo hivyo vikiendelea katika jamii, hususan ya waafrika waishio kusini mwa jangwa la sahara.

Umoja wa Mataifa na wadau wamekuwa wakihimiza serikali, asasi za kiraia na jamiikuondokana na imani hizo potofu na kuthamini maisha ya kila mtu. 

Sauti
4'20"

Nafurahia kuwa na ulemavu, kama si hilo nisingalikuwa mbunge-Sankok

‘Nafurahia kuwa na ulemavu’! Ni nadra sana kutarajia kusikia kauli kama hiyo kutoka kwa mtu yeyote hususan mtu anayeishi na ulemavu lakini kwake Mbunge mteule David Ole Sankok kutoka Kenya, kauli hiyo anairudia mara kwa mara. Bwana Sankok ambaye alipata ulemavu wa viungo kufuatia kuchomwa sindano akiwa mtoto mdogo iliyomlemaza anasema hali yake ameikubali na hata kujivunia kwani ilimchochea kufikia alipofika maishani licha ya hali yake na kwamba anatoka katika jamii ya watu wa asili, waMaasai nchini Kenya.

Sauti
3'50"
Picha: Kwa hisani ya James Waikibia

Madhara ya mifuko ya plastiki ni gharama kubwa kwa wakaazi Bujumbura

Mifuko ya plastiki imekuwa kero kwani ina madhara makubwa siyo tu kiafya bali pia kimazingira. Imesababisha kuziba kwa mifereji ya majitaka na huko kwenye maji  ikiathiri pia viumbe vya majini. Barani Afrika kuna nchi ambazo zimepitisha sheria kutokomeza matumizi ya mifuko ya plastiki kwa mfano Kenya na Rwanda na nyingine zikiweka mikakati kufikia hilo.

Sauti
4'26"
UN

Kilimo hai na nuru huko Gabon

Uhifadhi wa mazingira unakwenda sambamba na kilimo bora kinachohakikisha kuwa wakulima hawakwatui hovyo ardhi na hivyo kusababisha mmomonyoko wa udongo. Kama hiyo haitoshi, wakulima huelekezwa jinsi ya upanzi bora wa mbegu kuhakikisha kuwa wanapopalilia, basi wanahifadhi pia udongo. Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO limechukua hatua hiyo huko Gabon ambako jiwe moja limeua ndege watatu.

Sauti
4'

Je Tanzania ya kijani inawezekana? Dk Mwakaluka

Umoja wa Mataifa na wadau mbalimbali wamekuwa mstari wa mbele katika uhifadhi wa mazingira ili kubabiliana na tatizo la  tabianchi. Kampeni moja wapo katika ulinzi wa mazingira ni uhifadhi wa misitu ya asili na pia upandaji miti ili kufukia lengo la Umoja wa Mataifa la kuongeza misitu yote ya dunia  kwa asilimia  3 ifikapo mwaka 2030.

Sauti
3'59"
Picha ya UN /Manuel Elias

Upendo wa kweli sio lazima utoke kwa ndugu wa damu

Jumuiko la vijana mwaka huu katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, UN, lilisheheni shughuli mbalimbali zikiwemo mdahalo wa vijana na viongozi waandamizi wa UN, maonyesho na burudani kutoka kwa waimbaji mbalimbali.

Miongoni mwao ni Emmanuel Kelly ambaye ni mlemavu wa viungo, na mmoja kati ya vijana waliohutubia kwenye mkutano huo alikuwa kivutio kikubwa  wakati alizungumzia mambo mbalimbali kuhusu safari ya maisha yake binfasi .

Sauti
4'29"
Picha ya UN

Michezo ni daraja hata katika vita dhidi ya utumikishaji watoto

Katika kampeni ya kupiga vita utumikishwaji  wa watoto  kama askari katika maeneo ya migogoro ya vita inayoendeshwa na  shirika la Umoja wa Mataifa  la kuhudumia watoto UNCEF, imeamua kugeukia michezo kufikisha ujumbe kutokana na uwezo wa michezokuunganisha watu.Uwakilishi wa Ujerumani kwenye Umoja wa Mataifa ukaongeza nguvu katika kampeni hiyo kwa kuwaalika magwiji wastaafu wa kandanda waliowahi kuichezea ligi ya soka ya Ujerumani au  Bundesliga  kuja Umoja wa Mataifa kushiriki mechi kwa lengo la kuchagiza

Sauti
4'40"