Ukatili dhidi ya wakawake marufuku Burundi: Seruka
Ukatili wa kijinsia ni changamoto kubwa nchini Burundi huku Zaidi ya asilimia 90 ya wanaotendewa ukatili huo wakiwa ni wanawake na watoto. Sasa shirika lisilo la kiserikali la SERUKA limeamua kushikia bango dhuluma hiyo kwa kuendesha kampeni katika maeneo mbalimbali nchini humo kupinga na kuelimisha jamii kuachana na ukatili dhidi ya wanawake. Mwandishi wetu wa maziwa makuu Ramadhan Kibuga alitembelea moja ya kampeni za shirika hilo kwenye uwanja wa Parke mjini Bujumbura uangana naye kwenye Makala hii.