Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanawake lazima wapewe kipaumbele kutimiza ajenda ya 2030

Wanawake lazima wapewe kipaumbele kutimiza ajenda ya 2030

Pakua

Mashirika ya misaada ya kibinadamu, asasi za kiraia na serikali mbalimbali zimehimizwa kuwekeza nguvu zao katika kuinuwa vipato vya watu vijijini hususani wanawake kwa kupitia miradi ya ujasiriamali ,kutoa  mafunzo, semina na mbinu mbalimbali zitakazoliwezesha kundi hilo katika jamii.

Kwa kulitambua hilo huko nchini Pakistan  shirika la kazi duniani ILO kwa ushirikiano na serikali ya Canada wameanzisha kampeni ya usawa kijinsia kwa wanawake vijijini kwa kutoa elimu na mafunzo  ya ujasiriamali ili waweze kujikwamua na umasikini. Nini  kilichojiri huko? Ungana na Patrick Newman katika Makala hii upate undani…

Photo Credit
Wanawake wajasiriamali Pakistan. Picha: © ILO/A. Memon 2015