25 MACHI 2024
Hii leo jaridani mwenyeji wako ni Anold Kayanda akianzia na siku ya kimataifa ya kukumbuka watumishi wa UN wanaoshikiliwa vizuizini na wasiofahamika waliko, kisha anakwenda Sudan Kusini na harakati za kusaidia manusura wa ukatili wa kingono. Makala ni harakati za kumkomboa mwanamke na mashinani arejea Sudan Kusini.
22 MACHI 2024
Hii leo jaridani ikiwa ni Siku ya maji duniani, tunaangazia utunzaji wa vyanzo vya maji. Pia tunamulika mkutano wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW68 ambao umekunja jamvi hii leo. Makala tuankupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Tanzania kufuatilia jinsi ambayo miradi ya maji inavyoleta manufaa kwa jamii.