Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UNOG

Kilele cha haki za binadamu na uchambuzi wa ibara ya 30!

Leo ni siku ya haki za binadamu duniani ambapo ni kumbukizi ya miaka 70 tangu kupitishwa kwa tamko hilo tarehe 10 mwezi desemba mwaka 1948  huko Paris Ufaransa.

Miaka 70 iliyopita tamko la haki za binadamu lilipitishwa, ikiwa ni  baada ya vita vikuu vya pili vya dunia.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake anasema kuwa kwa miaka 70, tamko la kimataifa la Haki za Binadamu limekuwa ni mhimili wa kuangaza masuala ya utu, usawa na ustawi na kuleta mwangaza wa matumaini mahala penye giza.

Sauti
1'44"
FAO/Giulio Napolitano

Mauritius yaendelea kupanua wigo wa biashara mtandaoni, yaipiku Nigeria na Afrika Kusini

Mauritius imechukua nafasi ya juu kwa nchi za bara Afrika zenye utayari wa kufanya biashara kwa njia ya mitandao.

 Taarifa hizo zimetolewa leo kwenye ripoti ya Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo, UNCTAD mwaka ya mwaka 2018 kuhusu biashara mtandaoni, wakati huu ambapo mkutano wa siku tano kuhusu biashara mtandaoni barani Afrika ukianza leo mjini Nairobi Kenya.

 

Sauti
2'20"
ILO/Deloche P

Kigeugeu kwenye mkataba wa kimataifa wa uhamiaji ni taswira mbaya kwa nchi husika:Abour

Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya uhamiaji wa kimataifa  Louise Abour amesema dhamira iliyowekwa bayana na nchi kadhaa ikiwemo Hungary, Poland , Jamhuri ya Czech na Australia ya kujiengua kwenye mkataba wa kimataifa wa wahamiaji inaonyesha picha mbaya kwao na ina athari kubwa katika ari ya ushirikiano wa kimataifa . 

Sauti
3'23"
WFP/Jonathan Dumont

Serikali zina wajibu kuhakikisha wananchi wana makazi yenye staha.

Katika uchambuzi wa ibara kwa ibara za tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa, hii leo Assumpta Massoi anamulika ibara ya 15 ambayo inagusia haki ya msingi ya mtu kuishi maisha ya staha. Ibara hii inazingatia  ukweli kwamba baadhi ya maeneo licha ya sheria kutambua haki hiyo, bado maisha ya wananchi ni magumu, wakiishi maeneo yasiyo na staha, huduma za kijamii zikiwa ni mashakani. Na wakati mwingine, hata pale ambapo wananchi wamejinasua, wanakumbwa na ubomoaji ambao husababisha watumbukie tena kwenye mkwamo .Je hali inakuwa vipi na Umoja wa Mataifa unasema nini?

Sauti
3'22"

03 Disemba 2018

Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa leo Siraj Kalyango anaangazia

-Kuanza kwa mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya tabia nchi COP 24, Umoja wa Mataifa ukihizima ufadhili na kasi ya kupambana na mabadiliko hayo

-Siku ya Kimataifa ya watu wenye ulemavu , je ni yapi yanayomkabili mtu anayeishi na ulemavu? tutabisha hodi Kagera Tanzania

-Ngozi ya samaki aina ya sangara mali kubwa nchini Kenya kulikoni

-Makala tunaendelea na ibara za tamko la haki za binadamu leo ni ibara ya 23 ikiangazia haki za wafanyakazi wa ndani

Sauti
14'42"

29 Novemba 2018

Leo katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa Arnold Kayanda anakuletea

-Hatari ya VVU kwa vijana barubaru ifikapo 2030, barubaru 80 watapoteza maisha kila siku kama mwenendo hautobadilika limeonya shirika la UNICEF

-Umuhimu wa ushirika wa Kusini-Kusini kwa bara la Afrika ni mkubwa

-UNMISS kuongeza vikosi jimbo la Nile Sudan Kusini kwa ajili ya ulinzi wa raia

-Makala inamulika Ibara ya 21 ya tamko la haki za binadamu kuhusu "haki ya wananchi kushiriki katika serikali , huduma za jamii na uongozi kuzingatia matakwa ya wananchi".

Sauti
14'4"