Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

FAO/Olivier Asselin

Ukosefu wa elimu watumbukiza wengi kwenye ajira zisizo rasmi- Ripoti

Watu bilioni 2 kote ulimwenguni wanafanya kazi katika sekta isiyo rasmi na idadi kubwa ni katika nchi zinazoendelea na zile zinazoibuka kiuchumi.

 

Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya shirika la kazi duniani, ILO iliyochapishwa hii leo ikijikita katika takwimu za wanawake na wanaume walio kwenye sekta hiyo.

 

Ripoti inasema idadi hiyo ni zaidi ya asilimia 61 ya watu wote walioajiriwa duniani ikitanabaisha kuwa kiwango kidogo cha elimu ni kichocheo cha watu kuingia kwenye sekta hiyo.

 

Sauti
1'6"
Picha: UNPA

Muziki wa Jazz huleta amani-Hancock

Leo ni siku ya kimataifa ya muzizki wa Jazz, na maadhimisho ya kimataifa mwaka huu yanafanyika St. Petersburg, Urusi.

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO linasema wasanii zaidi ya 30 wamekusanyika St. Petersburg kusherehekea siku hiyo kwa kutoa burudani katika tamasha maalumu akiwemo  Luciana Souza.

UNESCO inaamini kwamba siku ya kimataifa ya jazz inaimarisha mawasiliano na utangamano katika jamii na lengo lake ni kuchagiza uhuru, ubunifu, majadiliano na kuunganisha watu kutoka kila kona ya duniani.

Sauti
1'39"
UNHCr/Anthony Karumba

UN na wadau waleta matumaini kwa watoto wakimbizi Rwanda

Watoto wakimbizi nchini Rwanda sasa wanaona nuru katika maisha yao kutokana na ushirikiano kati ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na mfuko wa H&M. 

Ubia huo unawezesha watoto wakimbizi nchini Rwanda kupata elimu kwa kuwa wanaishi katika makazi salama na zaidi ya yote wanapatiwa vifaa vya shule na kuwa na uhakika wa maisha yao ya baadaye.

Miongoni mwa wanufaika wa ushirika huo ni mwanafunzi Godfried kutoka Burundi ambaye sasa anaishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Mahama nchini Rwanda.

Sauti
1'22"
Maria Morera

Watu millioni 15 waliuzwa utumwani zaidi ya miaka 400 iliyopita

Mkutano huo wa video ulikuwa na kauli mbiu ya : kumbuka utumwa, vita na ushindi kupigania uhuru na usawa na kitovu cha mdahalo huo kilikuwa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York nchini Marekani  ambapo,  miongoni mwa wanafunzi waliounganishwa moja kwa moja na mkutano wa New York kupitia video ni wanafunzi wa Mexico pamoja na Tanzania. Baadhi ya walioshiriki wanaeleza jinsi mdahalo ulivyokwenda akianza Hussein Hamis kutoka shule ya upili ya Azania.

(SAUTI ZA WANAFUNZI TZ)

Sauti
2'4"
UNHCR/Achilleas Zavallis

Evros huko hali si shwari kwa wajawazito wakimbizi

Umoja wa Mataifa umeisihi Ugiriki iboreshe mazingira na kasi ya mapokezi ya wasaka hifadhi kwenye mkoa wa Evros ambako wakimbizi wanazidi kumiminika wakipitia mpaka wa nchi hiyo na Uturuki.

 

Yaelezwa kuwa mwezi huu pekee watu 2,900 wameingia Evros wengi wao wakiwa ni wanafamilia kutoka Syria na Iraq, idadi ambayo inaelezwa ni nusu ya watu wote walioingia eneo hilo mwaka jana.

 

Sauti
1'31"
UN News

Mila zetu za umiliki wa ardhi ndio muarobaini wa mivutano- Jamii ya asili

Jukwaa la kudumu la watu wa asili la Umoja wa Mataifa linakunja jamvi leo Ijumaa huku washiriki wakiweka msisitizo suala la kujumuisha sheria za umiliki wa ardhi za kimila ili kuepuka mizozo ya umiliki wa ardhi za watu wa jamii hiyo.

 

Akihojiwa na Idhaa ya UN kando ya jukwaa hilo, Dk Elifuraha Laltaika, ambaye ni mtaalamu huru wa jukwaa hilo amesema msisitizo huo unazingatia kwamba..

 

(Sauti ya Dkt. Elifuraha Laltaika)

 

Sauti
1'37"