UN na fursa ya kuleta nuru Hodeidah
Matukio kwenye uwanja wa vita ni kikwazo kwenye mchakato wa amani nchini Yemen, lakini mazungumzo ya kisiasa ni kipaumbele cha juu cha kutatua mgogoro huo, amesema mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen katima mahojiano maalum na Idhaa ya Umoja wa Mataifa.
Bwana Griffiths amesema kuwa kipaumbele kikuu na cha juu ni kuwezesha mazungumzo ili kukomesha vita akisema kuwa “Hodeida ni suala la kipekee na muhimu, lakini si muhimu zaidi kuliko suala la suluhisho la kisiasa."