Wanawake wametaabika sana mwaka 2020:UNFPA
Mwaka 2020 ukielekea ukingoni, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya idadi ya watu, UNFPA, Dkt. Natalia Kanem amesema mwaka huu wa 2020 ulikuwa ni mwaka wa janga kuu zaidi kwa wanawake na wasichana ambao tayari walikuwa kwenye masahibu hata kabla ya janga hilo.