Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Rohingya

Wasichana wadogo katika kambi ya wakimbizi wa ndani nchini Myanmar wanachota maji kutoka kwenye kisima.
UNOCHA/Z. Nurmukhambetova

Nasimama katika mshikamano na watu wa Myamnar : Guterres

Ikiwa hapo kesho Jumanne, Februari 1,2022 ni maadhimisho ya mwaka mmoja tangu jeshi la Myanmar kupindua Serikali ya kiraia iliyochaguliwa kwa njia ya kidemokrasia na kuwaweka kizuizini kiholela viongozi wa Serikali, akiwemo Mshauri wa Serikali Aung San Suu Kyi na Rais Win Myint. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema anasimama katika mshikamano na watu wa Myanmar na matarajio yao ya kidemokrasia kwa jamii jumuishi na ulinzi wa jamii zote, ikiwa ni pamoja na Rohingya.

Mkimbizi wa ndani nchini Msumbiji akipokea msaada wa chakula
© WFP/Grant Lee Neuenburg

Kuisaidia WFP ni kuwasaidia wakimbizi kama Adu

Mkimbizi wa ndani Abbas Adu na wengine 400,000 wamelishukuru Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula WFP kuwapatia msaada wa chakula wakati huu ambapo WFP imepaza sauti kwa wahisani kusaidia wananchi Milioni 41 wanaokabiliwa na njaa kutokana na hali mbaya ya hewa ambayo imeathiri mavuno yao na hivyo kukosa chakula.

Sauti
2'2"