Kuwa mkimbizi sio kukosa matumaini kwa wanawake wa Rohingya: UNHCR
Maelfu ya wanawake wa Rohingya waliokimbia machafuko nchini Myanmar na kupata hifadhi ya ukimbizi Bangladesh, sasa wameanza kuona nyota ya jaha baada ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR kuwapa mafunzo ya ufundi cherahani.