Türk apendekeza mbinu iliyoratibiwa ili kuwaokoa Warohingya baharini
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk leo jijini Geneva, Uswisi ametoa wito wa kuwepo kwa mbinu iliyoratibiwa ya kikanda ili kuwalinda maelfu ya Warohingya waliokata tamaa wanaohatarisha maisha yao kwa kufanya safari hatari za baharini.