Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Mradi wa FAO nchini Thailand wa kupunguza upotevu wa chakula na taka kuna jukumu muhimu katika kubadilisha mifumo ya kilimo na chakula.
© FAO/Alisa Suwanrumpha

Mradi wa FAO wa kupunguza upotevu na utupaji wa chakula nchini Thailand wainua kipato cha wafanyabiashara

Kupunguza upotevu na utupaji wa chakula kuna jukumu muhimu katika kubadilisha mifumo ya kilimo na chakula. Kati ya malengo 17 ya Maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa ambayo yanafikia kilele mwaka 2030 lengo namba 2 linahimiza kutokomeza njaa, lengo namba 8 linahimiza kazi nzuri na ukuaji wa kiuchumi na lengo namba 12 lina himiza utumiaji na uzalishaji wenye kuwajibika lengo likiwa kuwa na mifumo endelevu ya utumiaji wa rasilimali. Malengo yote haya yanaenda sambamba na harakati za kupunguza upotevu na utupaji wa chakula.