Fahamu kuhusu Jukwaa la vijana ya UN
Vijana ni mawakala wa thamani wa mabadiliko na duniani kote wanachukua mambo mikononi mwao na kupigania suluhu za kibunifu ili kuharakisha utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu
(SDGs).
Vijana ni mawakala wa thamani wa mabadiliko na duniani kote wanachukua mambo mikononi mwao na kupigania suluhu za kibunifu ili kuharakisha utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu
(SDGs).
Walezi, viongozi wa afya na wahudumu wa afya wa jamii wanaojitolea wanatafakari juu ya utekelezaji wa chanjo ya malaria na jinsi nyenzo hiyo mpya inavyowafikia watoto walio hatarini kwa kuzuia malaria kuokoa maisha.
Huku uchumi wa dunia ukiendelea kuathiriwa na mfululizo wa migogoro, maafisa wakuu wa Umoja wa Mataifa na wawakilishi wa serikali wanakutana kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani, katika jaribio la kubadilisha mfumo wa fedha wa kimataifa, na kurejesha ajenda ya maendeleo endelevu ya 2030 iliyokubaliwa kimataifamkwenye mstari unaostahili.
Ugonjwa wa chikungunya kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO ni ugonjwa unaonezwa na mbu jike aina ya Aedes aliyebeba virusi vya chikungunya. WHO kupitia ukurasa wake wa kuchambua magonjwa inasema kuna spishi mbili za Aedes zinasambaza ugonjwa huo ambazo ni Aedes aegypti na Aedes albopictus. Spishi hizi mbili zinaweza pia kusambaza magonjwa mengine yanayoenezwa na kama vile dengue. Mbu hawa hung’ata nyakati za mchana, ingawa wanaweza pia kung’ata asubuhi na alasiri.
Hii leo ni siku ya kimataifa ya kuendeleza utamaduni wa amani, upendo na dhamiri na hii inatokana na azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa namba A.73/101 lililopitishwa tarehe 29 mwezi Julai mwaka 2019 jijini New York, Marekani.
Hivi karibuni shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa duniani, WMO kupitia kamati yake inayosimamia masuala ya vimbunga liliondoa katika orodha ya vimbunga ya kitropiki kwenye bahari ya Atlantiki majina Fiona na Ian. WMO kupitia taarifa yake hiyo iliweka bayana sababu za uamuzi huo kuwa ni madhara makubwa yaliyosababisha vimbunga hivyo huko Amerika ya Kati, Karibea, Marekani na Canada