Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UNnewskiswahili/Patrick Newman

Mtazamo wa jamii kuwa mwanamke kiongozi ametelekeza familia unasikitisha- Gavana Laboso

Mtazamo potofu wa jamii ya kwamba mwanamke anayejishughulisha na masuala ya uongozi hususan wa kisiasa hajali familia yake au hawezi kutunza familia  hiyo ni wa kusikitisha Hiyo ni kauli ya Joyce Laboso, gavana wa kaunti ya Bomet nchini Kenya, akisema mtazamo huo na changamoto zingine zinaathiri ushiriki wa wanawake katika uongozi hususan siasa.

Sauti
3'57"
UN News Kiswhaili/Patrick Newman

Teknolojia ya asili ya wafugaji inasaidia mnepo wa mabadiliko ya tabianchi:TANIPE

Changamoto za mabadiliko ya tabianchi kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa hazichagui wala hazibagui taifa au jamii utokayo zinamuathiri kila mtu duniani na ndio maana wito unatolewa kila uchao kuchukua hatua zote stahiki kujenga mnepo dhidi ya zahma hiyo kote duniani. Wito huo hivi sasa unaitikiwa sio tu na serikali mbalimbali kuweka será na mikakati , bali pia wadau wote wakiwemo asasi za kiraia ,sekta binafsi, jamii na hata mashirika ya kijamii.

Sauti
5'15"
Picha na UNICEF/UNO72220/Phelps

Je wafahamu kuna vazi linaloweza kukuepusha na Malaria ?

Kila uchao harakati zinaendelea ili kuhakikisha kuwa ugonjwa wa Malaria uliosababisha vifo vya watu zaidi ya 400,000 mwaka 2017 unatokomezwa duniani kote. Hali ya ugonjwa  huo ni mbaya zaidi katika nchi 11 ambazo Burkina Faso, Cameroon, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRc, Ghana, India, Mali, Msumbiji, Niger, Nigeria, Uganda na Tanzania. Serikali, mashirika na taasisi za kiraia zinabonga bongo kuibuka na mkakati wa kuondokana na ugonjwa  huo unaozuilika ambapo mbinu ya karibuni zaidi ni ile ya kutengeneza vazi ambalo kwamo katu mbu anayeeneza ugonjwa wa Malaria hawezi kusogea.

Sauti
4'13"
UN Photo/John Robaton

Juhudi za kukabiliana na mihadharati zaimarishwa kunusuru vijana, Uganda.

Umoja wa Mataifa, wadau wake pamoja na nchi wanachama wa Umoja huo kote duniani bado wanaendelea na harakati za kuhakikisha malengo 17 ya maendeleo endelevu yanafikiwa ifikapo mwaka 2030.

Lengo namba tatu linazungumzia afya bora na ustawi wakati lile la namba nne linazungumzia elimu bora. Hatua zimepigwa kufikia sasa katika kuyafanikisha malengo hayo lakini ni dhahiri kuwa bado safari ni ndefu kwani  nchi zinakutana na vikwazo mbalimbali ikiwemo athari za biashara na matumizi ya dawa za kulevya hususan kwa vijana.

Sauti
3'55"
UN

Nguva warejea Madagascar, ni baada ya wananchi kuchukua hatua

Uharibifu wa mazingira unazidi kutishia siyo tu uhai wa binadamu bali pia viumbe vingine vinavyoishi nchi kavu na hata baharini. Miongoni mwa viumbe vilivyo hatarini ni nguva ambao uwepo wao baharini unasaidia kumea kwa mimea ya baharini iliyo muhimu kwa chakula cha samaki. Ni kwa kuzingatia hilo Umoja wa Mataifa kupitia lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linatilia mkazi uhai wa viumbe vilivyo chini ya maji, ikiwemo baharini. Nchini Madagascar, kuongezeka kwa idadi ya watu kunatia shinikizo kwenye mazingira na nguva wako hatarini.

Sauti
3'50"
UNHCR/Catherine Wachiaya

Walimu wa Kiswahili wamekiri kitabu changu kiliwashawishi kuthamini lugha hiyo adhimu- Walibora

Shirika la elimu sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa, UNESCO limekuwa katika mstari wa mbele katika kuchagiza kuwepo kwa dunia yenye watu wanaojua kusoma na kuandika. UNESCO kwa mtazamo wake unachukulia kupata stadi na kuimarisha stadi hizo za kusoma na kuandika katika maisha kama sehemu muhimu ya haki ya elimu. Matokeo yake yakiwa ni kuwawezesha watu kushiriki kikamilifu katika jamii na kuchangia katika kumarisha maisha yao.

Sauti
4'6"
UN SDGs

Vijana Tanzania msisalie watazamaji wa harakati za maendeleo, jumuikeni- Mulika

Umoja wa Mataifa kupitia malengo ya maendeleo endelevu, SDGs au ajenda 2030 unataka serikali, mashirika na asasi mbalimbali kuhimza jamii ulimwenuni hususan vijana  kushiriki kikamilifu katika miradi mbalimbali  ya kimaendeleo ili kuweza kufikia malengo hayo ifikapo mwaka 2030.

Vijana ambao ndio wameshika usukani wa mustakabali wa dunia wanachagizwa kusaka na kutumia fursa za kimaendeleo ili kuweza kujikwamua na changamoto zinazowakabili ikiwemora ajira.

Sauti
4'2"
World Bank/Arne Hoel

Wanaume Uganda wafunguka kuwezesha wake zao.

Kuna msemo ukiwezesha mwanamke unawezesha jamii, ingawa mzigo huo wa kumwezesha mwanamke mara nyingi umekuwa hautiliwi maanani na wananaume hususan katika kuwawezesha wake zao.


Lakini hali ni tofauti kwa Anthony Kiiza wa mjini Hoima ambaye amewezesha mkewe kwa kutumia ufadhili chini ya mradi wa serikali wa kuwezesha vijana wa Youths Livelyhood Programme.

Je, kuna manufaa ya mwanamume kushirikisha mkewe katika mipango ya maendeleo? Ungana na John Kibego katika Makala ifuatayo.

 

Sauti
3'23"
FAO/Riccardo Gangale

FAO yapatia wakulima 200,000 Kenya stadi za kuhimili mabadiliko ya tabianchi

Nchini  Kenya mabadiliko ya tabianchi yamesababisha Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na serikali kusaidia wakulima, wafugaji na wavuvi kuweza kupata stadi mpya ili hatimaye waweze kunufaika na ufugaji, kilimo na uvuvi. Umoja wa Mataifa umechukua  hatua  hiyo kwa kutambua kuwa mabadiliko ya tabianchi yasiposimamiwa vyema yatasababisha umaskini kuongezeka sambamba na ukosefu wa chakula. Mathalani wakulima waliozoea kulima kwa kutegemea misimu ya hali ya hewa hivi sasa wamevurugwa kwa kuwa misimu hiyo haitabiriki tena.

Sauti
4'6"