Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

©FAO/Laure-Sophie Schiettecatte

Uendelevu wa uhakika wa chakula wamulikwa, Uganda

Ukosefu wa uhakika wa chakula na lishe hutokea wakati watu wanakosa fursa ya kuchagua, wanakuwa na wasiwasi kuhusu kuishiwa na chakula na wanalazimika kubadilisha ratiba ya kupata mlo kwa sababu za kiuchumi.

Kwa mujibu wa shirika la chakula Na kilimo duniani, FAO, hili linaweza kutokana na umaskini, mazao duni au mabadiliko ya tabianchi. FAO inasema ili kufikia uhakika wa chakula inamaanisha kupata chakula bora na endelevu na kwa viwango sahihi kwa ajili ya watu katika kaya.

Sauti
3'47"
UNIC/Stella Vuzo

Mahojiano yangu na Idhaa ya Kiswahili ya UN yamenifungulia njia: Kijana Idd

Dunia imeendelea kukumbwa na majanga yanayosababishwa na mabadiliko ya tabianchi. Kwa mujibu wa utafiti wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira UNEP kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya mabadiliko ya tabianchi na uharibifu wa mazingira kama ukataji miti hovyo.

Ni katika kipindi hiki ambapo kote duniani kila mtu anahamasishwa popote pale alipo afanye lolote awezalo ili kudhibiti mabadiliko ya tabianchi kama vile ongezeko la joto duniani au baridi kali   vitokanavyo na uharibifu wa mazingira.

Sauti
3'59"
UNICEF/Prashanth Vishwanathan

Likizo ya uzazi ni haki ya mama na mtoto: Doris Mollel

Likizo ya uzazi ni haki kwa kila mama anayefanyakazi kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa na ni muhimu katika afya ya mama na mtoto lakini zaidi ukuaji wa mtoto. Hata hivyo kwa mujibu wa shirika la kazi duniani , ILO lililopisha mkataba wa likizo ya uzazi mwaka 1919, suala hili limekuwa changamoto kwa mamilioni ya wazazi katika nchi nyingi duniani kutokana na sheria za kazi zilizowekwa na waajiri wao.

Sauti
5'36"
UNDP Tuvalu/Aurélia Rusek

Wanajamii wana majibu sahihi kuhusu changamoto za uharibifu wa mazingira- Dkt Elifuraha Lalitaika.

Kila uchao ripoti za watu wa asili kufurushwa kwenye maeneo yao ya asili kwa sababu ya kuimarisha uhifadhi wa mazingira au kuepusha watu wa jamii hizo kuharibu maeneo hayo, zimekuwa zikisika. Matukio haya ni kuanzia Afrika hadi Ulaya, Amerika hadi Asia bila kusahau Amerika ya Kusini. Katika maeneo mengine, watu hao hufurushwa kwa ajili ya kufanikisha miradi inayodaiwa kuwa ni ya maendeleo huku watu wa jamii ya asili wakisalia bila mazingira ambayo wamezoea.

Sauti
3'42"
UNICEF/Frank Dejongh

Wadau mkoani Ruvuma nchini Tanzania na harakati za kusongesha afya ya mtoto

Shirika la afya duniani, WHO, linasema upatikanaji wa huduma ya afya ni changamoto katika mataifa mengi hususan yanayoendelea na hivyo ni muhimu kwa serikali na wadau kushirikiana katika kuhakikisha huduma hiyo inapatokana hasa kwa watoto. Tanzania ni miongoni mwa nchi hizo zinazoendelea zinazojaribu kutumia mbinu mbalimbali kukabiliana na changamoto hizo za afya hususan kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu je nini kinafanyika?

Sauti
5'18"
IOM/A. Deng 2018

Lugha ya kityaba iko hatarini kupotea nchini Uganda

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya lugha ya mama hii leo Umoja wa Mataifa umesema lugha na utofauti wake wa utambulisho, kuwasiliana, kushirikiana kijamii, elimu na maendeleo ni muhimu kwa ajili ya binadamu na sayari dunia. Hatahivyo kukua kwa utandawazi kumesababisha lugha nyingi kuwa hatarini kupotea na iwapo lugha inapotea basi utofauti wa utamaduni unapotea na hivyo kuathiri kiungo muhimu cha jamii hizo. Nchini Uganda lugha ya kityaba inakabiliwa na hatari hii ambapo jamii wenyeji wa lugha hiyo wanahofu kubwa na lugha yao, kulikoni?

Sauti
3'45"
© UNICEF/Pirozzi

Kijana mwanafunzi  Tanzania aanzisha klabu kuwasaidia wanafunzi wasioona wafurahie haki ya elimu 

Leo Februari 20 ni siku ya kimataifa ya haki za kijamii ikibeba kauli mbiu, ukitaka amani na maendeleo fanyia kazi haki za kijamii. Umoja wa Mataifa umesema haki hizi ni muhimu kwa ajili ya kuishi kwa amani na maendeleo. Haki za kijamii zinaendelezwa pale vikwazo ambavyo watu wanakumbana navyo kwa misingi ya jinsia yao, umri, rangi, dini , utamaduni au kuishi na ulemavu.

Sauti
4'1"
FAO/Giulio Napolitano

Biashara ya mtandao yasaidia kuinua kipato cha mwanamke mjasiriamali Burundi

Mchango wa wanawake ni muhimu katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, ambamo usawa wa kijinsia ni miongoni moja ya malengo hayo hatahivyo ufiaji wake bado ni changamoto.

Kwa mujibu wa shirikla la Umoja wa Mataifa linalohusika na maswala ya wanawake, UN Women kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake ni muhimu kwa kila lengo na kwamba haki hizo zitaweza kustawisha jamii, katika nyanja mbali mbali ikiwemo kiuchumi.

Sauti
3'52"
UNAMID/Albert González Farran

Mabadiliko ya tabianchi yameathiri wote ikiwemo wafugaji- Bi Leina

Jamii za wafugaji ni kundi ambalo namna ya kujipatia kipato inategemea mifugo na mifugo inatagemea lishe ambayo uwepo wake hivi sasa unakumbwa na madhara ya mabadiliko ya tabianchi. Madhara ya aina hiyo yamesababisha wanaharakati kujitokeza kuhakikisha kuwa ufugaji unaendelea na mifugo inapata malisho bora. Nchini Kenya Agnes Leina ambaye ni mwanzilishi wa shirika lisililo la kiserikali la Illaramatak Community Concerns linalenga jamii za wafugaji. Kwa mujibu wa Bi.

Sauti
3'25"