Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Afisa Habari wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO ofisi ya Beni jimboni Kivu Kaskazini akipatia mafunzo wanahabari, wanaharakati na wanafunzi wa Vyuo Vikuu kuhusu habari potofu na habari za uongo mjini Beni.
UN./George Musubao

MONUSCO imetuepusha kutumbukia kwenye usambazaji wa habari za uongo na potofu- Wanufaika

Kesho nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ni uchaguzi mkuu ikiwa ni tamati ya kampeni huku Umoja wa Mataifa kupitia ujumbe wake wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umeshiriki kwa kusafirisha sio tu vifaa vya uchaguzi lakini pia kuelimisha wananchi jinsi ya kukabili na kuzia habari potofu na za uongo kwani ni tisho la amani na usalama. 

Lilly Kiden akibeba mazao ya mbogamboga kutoka kwa shamba lake.
FAO

Asante FAO kunijengea mnepo sasa najikimu mimi na familia yangu: Lilly Kiden

Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP28 ukijiandaa kufunga pazia hapo kesho nakupeleka Sudan Kusini jimbo la Equatorial Mashariki ambako wakulima walioathirika na mabadiliko ya tabianchi sasa wanajengewa mnepo na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na wengi wameweza kujikwamua pamoja na familia zao. Ungana na Flora Nducha akikuletea safari ya mafanikio ya mmoja wa wanuafa wa mradi huo wa FAO. 

Sauti
2'8"
Kiwanda cha uzalishaji wa nishati ya jua kata kisiwa cha Unguja nchini Tanzania.
World Bank

Benki ya Dunia yasaidia ukuzaji wa rasilimali watu na maendeleo nchini Tanzania

Tarehe 19 Desemba mwaka 2019, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio namba 74/245, ambalo liliteua tarehe 4 Desemba kuwa Siku ya Kimataifa ya Benki kwa kutambua mchango mkubwa wa benki za maendeleo za kimataifa na benki nyingine za maendeleo za kimataifa katika kuleta maendeleo endelevu na kuchangia uboreshaji wa hali za maisha za wananchi. 

Sauti
2'5"
Kikundi Cha Bendera cha Pamoja cha Walinda Amani wa Tanzani na Nepali wakitoa Salamu kwa Mkuu wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani DRC, MONUSCO.
MONUSCO

Walinda amani wa MONUSCO kutoka nchini Tanzania na Nepal watunukiwa Nishani

Vikosi vya Walinda Amani kutoka Tanzania Kwa kushirikiana Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa kutoka nchini Nepali wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemkorasia ya Kongo – DRC wamefanya gwaride la pamoja na kutunikiwa Nishani za Umoja wa Mataifa na Mkuu wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani DRC, MONUSCO Luteni Jenerali Otavio Miranda Filho ikiwa ni kuthamini mchango wao wa kuhakikisha Amani ya Kudumu na Usalama vinapatikana nchini DRC.