Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katika nyika za Kazakh, idadi ya saigas iliyowekwa kwenye orodha  nyekundu ya wanyama walio hatarini kupotea tayari imepita milioni 2.5.
Huduma ya vyombo vya habari ya Wizara ya Ikolojia na Maliasili ya Kazakhstan.

Kasi ya kutoweka viumbe hai imesababisha athari kubwa ya upotevu wa bioanuwai: UN

Ijapokuwa karibu aina milioni moja ya viumbe hai kwa sasa ziko katika hatari ya kutoweka, Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa UNU huko Bonn nchini Ujerumani kinatoa tahadhari ya "kutoweka kwa pamoja na athari zinazoingiliana zinatotokea wakati kuna kutoweka kabisa kwa aina moja kunakuathiri nyingine.

UNICEF na wadau wake wasaidia kaya zilizoathirika na mafuriko zinapokea kwa kwa kuwapa msaada wa fedha taslim kupitia M-pesa na vocha za kielektroniki ili kuweza kujikimu na kimaisha.
UNICEF

Msaada wa fedha toka UNICEF unatusitiri baada ya mafuriko: Waathirika Garisa Kenya

Kenya inashuhudia kiwango kikubwa cha mvua zaidi ya kile cha kawaida ambacho kimesababisha mafuriko makubwa, maporomoko ya udongo na maelfu ya watu kutawanywa hivi karibuni. Miongoni mwa maeneo yaliyoathirika zaidi ni Kaunti ya Garisa , ambako hivi sasa asante kwa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na wadau wake kama shirika la Norway kwa ajili ya ushirikiano wa maendeleo NORAD, Mamlaka ya Kitaifa ya kudhibiti Ukame Kenya NDMA, na serikali ya Kaunti ya Garasa  kwani kaya zilizoathirika na mafuriko zinapokea msaada wa fedha taslim kupitia M-pesa na vocha za kielektroniki ili kujikimu kimaisha.

Audio Duration
3'11"
Alice Wairimu Nderitu (kwenye skrini), Mshauri Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Kuzuia Mauaji ya Kimbari, akitoa taarifa kwa mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu ulinzi wa raia (PoC) katika vita zinazotumia silaha.
UN Photo/Eskinder Debebe

Mwaka 2023 mizozo ya kivita iligharimu maisha ya zaidi ya watu elfu 33

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya mkutano leo Jumanne Mei 21 kuhusu ulinzi wa raia katika vita, kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 25 tangu kupitishwa kwa azimio nambari 1265 (1999), ambalo lilibainisha ulinzi wa raia kama suala muhimu katika amani na usalama wa kimataifa, na Maadhimisho ya miaka 75 ya kupitishwa kwa azimio 1265 (1999) la Mkataba wa Geneva.