Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Husna Mbaraka, afisa msimamizi wa masuala ya ardhi, maliasili na jinsia wa FAO nchini Kenya akizungumza na Flora Nducha jijini New York Marekani.
UN News

Teknolojia inaleta tija kwa wanawake wakulima nchini Kenya: Husna- FAO

Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO nchini Kenya linafanya kila juhudi kuhakikisha linatimiza wito wa Umoja wa Mataifa wa kutaka ubunifu na teknolojia vitumike kama nyenzo ya kumuinua mwanamke  kiuchumi na kijamii lakini pia katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs na kuhakikisha hakuna anayesalia nyuma kwenye zama hizo za kidijitali.

Mkazi huyu wa Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC aitwaye Joel Methya Ndeku alipoteza ndugu zake katika mauaji ya mwaka 2018 na hadi leo hafahamu chochote kuhusu wauaji.
UN News/George Musubao

UN itusaidie tupate ukweli na haki kwa kuuawa kwa ndugu zetu – Mkazi Beni, DRC

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mashambulizi yanayoendelea mashariki mwa nchi hiyo kwenye jimbo la Kivu Kaskazini yanasababisha sio tu vifo bali machungu yasiyoisha kwa familia za waliouawa kwa kushindwa kufahamu ukweli wa nini kiliwafika jamaa zao, nani aliwaua, na haki gani imetendeka na sheria dhidi ya waliohusika. 

Sauti
4'16"
Naibu Meya wa Wilaya ya Musanze katika jimbo la Musanze nchini Rwanda akihojiwa na Assumpta Massoi wa Idhaa ya Kiswahili ya UN kando mwa mkutano wa Maji, jijini New York.
UN Video

Lengo langu ni kupata jawabu la teknolojia ya kusafisha maji eneo letu

Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu maji ukiingia siku ya tatu kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa huku moja ya mikakati ni kuhakikisha kunakuweko matumizi endelevu ya maji, mmoja wa washiriki kutoka Rwanda amezungumzia vile ambavyo teknolojia ya kusafisha maji taka ili yaweze kutumika tena na tena inaweza kuwa mkombozi kwenye eneo lao.

Sauti
4'7"
Sostine ambaye ni mchuuzi wa maji katika mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC anamweleza mwanahabari mtoto Liesse ya kuwa hulazimika kuweka dawa kwenye madumu ya maji kwa sababu maji ya Ziwa Kivu yana taka.
UNICEF VIDEO

UNICEF yawezesha wanahabari watoto kupasha umma kuhusu changamoto za maji DRC

Hii leo ni siku ya maji duniani na ninakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako huko mtoto Liesse mwenye umri wa miaka 17 amefuatilia upatikanaji wa maji safi ya kunywa kwenye eneo la Goma jimboni Kivu Kaskaizini baada ya kupatiwa mafunzo ya uandishi wa habari na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF na hatimaye taarifa yake kutangazwa na Radio Okapi ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo

Sauti
2'23"
Vakyeka Kaswera, mkazi wa mji wa Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
UN News/ George Paluku

Umoja wa Mataifa usaidie kuturejeshea furaha - Wakazi wa Beni, DRC

Leo ni siku ya furaha duniani ambapo Umoja wa Mataifa unasema ni siku ya kutabua umuhimu wa furaha kwa watu wote ulimwenguni kwani ni msingi wa lengo la ubinadamu na pia huchagiza ukuaji wa kiuchumi ambapo baadhi ya wakazi wa Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wameomba Umoja wa Mataifa uwasaidie kurejesha furaha kwani ukosefu wa amani  unawanyima furaha waliyokuwa nayo zamani.  

Sauti
3'9"
Elionora Emiel Wilfred, mwanafunzi wa kidato cha 4 katika shule ya sekondari ya Mtakatifu Thereza wa Avila mkoani Kilimanjaro nchini Tanzania akihojiwa na UN News Kiswahili service kandoni mwa mkutano wa CSW67 jijini New York Marekani.
UN News

Wasichana tujengewe uwezo wa teknoljia na tupatiwe haki yetu ya elimu bora – Elionora CSW67

Mkutano wa 67 wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW67 ukielekea tamati mwaka huu 2023 kikiwa kimebeba mada uvumbuzi, mabadiliko ya kiteknolojia, na elimu katika zama hizi za kidigitali kwa ajili ya kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake na wasichana wote, mijadala mingi ilijikita katika kuwawezesha na kuhakikisha watoto wa kike wanaingia kwenye masomo ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati au STEM ili hapo baadaye waweze kuchangia katika ubunifu wa teknolojia katika enzi hizi za dunia ya kidijitali.  

Sauti
5'25"