Mimi ni simulizi ya kupendeza-Doreen Moraa Moracha
Kuelekea siku ya UKIMWI duniani tarehe Mosi mwezi ujao wa Desemba, Doreen Moraa Moracha, msichana kutoka Kenya ambaye anaishi na virusi vya UKIMWI amekuwa changamoto kubwa katika kumaliza unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi au VVU.