Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wang Yi, waziri wa mambo ya nje wa Jamhuri ya watu wa China akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kikao cha 74
UN Photo/Loey Felipe

Asilani hatutotiwa woga na vitisho:China

Katika hotuba yake kwenye mjadala Mkuu wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa Diwani wa jimbo na waziri wa mambo ya nje wa Uchina ametangaza kwamba nchi yake asilani haitotiwa woga na vitisho au kukubali shinikizo wakati inapokabiliwa na changamoto za ulinzi.

Picha ya maktaba ikionesha wamisri wakiandamana mwezi Julai mwaka 2013
UN News Centre

Kamata kamata kufuatia maandamano Misri inatutia hofu kubwa:Bachelet

Kamishina mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet leo Ijumaa ameelezea wasiwasi mkubwa alionao kuhusu taarifa za kutokuwepo mchakato wowote kufuatia idadi kubwa ya kamata kamata ya watu ikihusishwa na maandamano nchini Misri, na kuutaka uongozi wa Misri kuheshimu haki ya uhuru wa kujieleza na kukusanyika kwa amani kwa kutekeleza kanuni na viwango vya kimataifa.