Tusaidie manusura na waathirika wa ugaidi angalau kupunguza makovu yao- Guterres
Leo ni siku ya kimataifa ya kumbukizi na kutambua waathirika na manusura wa vitendo vya ugaidi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumza kwenye tukio maalum lililofanyika katika makao makuu ya chombo hicho jijini New York, Marekani akisema kuwa ugaidi na aina zake zote umesalia changamoto kubwa.