Wengine wanaweza kusema huwezi kupambana na mabadiliko ya tabianchi na ukawa na uchumi mzuri. Ninakataa!-Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo akiwa mjini New York Marekani kabla ya kusafiri kwenda Argentina unakofanyika mkutano wa nchi 20 zilizoendelea zaidi kiuchumi G20, amewaambia wanahabari kuwa changamoto kubwa hivi sasa ni ukosefu wa kuaminiana duniani.