Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UNHCR imeitaka Uswis kutorejesha waomba hifadhi

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR leo limeiomba serikali ya Uswis kuhakikisha kwamba sheria za kutowarejesha kwa nguvu waomba hifadhi haziko hatarini hasa wakati huu ambapo kuna mjadala unaendelea wa kuwafukuza wageni ambao ni wahalifu.

Rais wa Uganda azuru Somalia na kuahidi kuisaidia nchi hiyo

Chini ya masaa ishirini na manne baada ua bunge la Somali kupiga kura ya kutokuwa na imani na baraza la mawaziri lililoteuliwa na waziri mkuu Mohamed Abdullahi Mohamed, rais wa UgandaYoweri Museven alifanya ziara mjini Mogadishu ambapo alikutana na mwenzake rais wa Somali Sharif Sheikh Ahmed, Spika wa bunge la Somali Sharif Hassan Sheikh Adan pamoja na waziri mkuu Mohamed Abdullahi Mohamed.

Mazungumzo ya amani ya Darfur yaanza tena:UM

Kundi la wapatanishi wakiwemo Umoja wa Mataifa , Muungano wa Afrika na Qatar wamewasili kwenye jimbo lililokubwa na mzozo la Darfur nchini Sudan wakati wa kuanza kwa mazungumzo yatayochukua siku kadha ya kuendeleza kupatikana kwa amani katika jimbo hilo.