UNHCR imeitaka Uswis kutorejesha waomba hifadhi
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR leo limeiomba serikali ya Uswis kuhakikisha kwamba sheria za kutowarejesha kwa nguvu waomba hifadhi haziko hatarini hasa wakati huu ambapo kuna mjadala unaendelea wa kuwafukuza wageni ambao ni wahalifu.