Nigeria yatakiwa kupambana na maambukizi ya HIV kutoka kwa mama hadi kwa mtoto
Mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya ukimwi UNAIDS Michel Sidibe yuko ziarani nchini Nigeria.
Mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya ukimwi UNAIDS Michel Sidibe yuko ziarani nchini Nigeria.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya haki za binadamu na uhuru wa watu wa jamii za kiasili, Prosefa S James Anaya leo ameitaka serikali ya Botswana kushughulikia kikamilifu masuala yanayozikabili jamii nyingi za watu asili (indigineous people).
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ametoa wito wa kuwepo na juhudi za pamoja ili kupambana na uhalifu. Akizungumza kwenye mjadala wa baraza la usalama kuhusu vitisho vya kimataifa dhidi ya amani na usalama , amekumbusha jinsi nchi wanachama walivyoungana kukabiliana na magonjwa, umasikini, mabadiliko ya hali ya hewa na ugaidi.
Mwakilishi maalumu wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya watoto na migogoro ya kutumia silaha Radhika Coomaraswamy katika kuhitimisha ziara yake ya siku sana nchini Afghanistan amesema kuwalinda watoto lazime kuwe ndio kitovu cha ajenda ya mapatano kama ilivyoidhinishwa na jamii ya kimataifa.
Mkurugenzi mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva amesema tusisahau ukweli kwamba kufuta hukumu ya kifo ni vigumu na ni mchakato nyeti kwa jamii nyingi.
Mkuu wa shirika la aya duniani WHO Margaret Chan ameonya kuwa kuna tatizo la magonjwa yasiyo ya kambukiza na tatizo lenyewe ni kubwa na huenda likaongezeka.
Mpangu wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika kwenye jimbo la Darfur Sudan umepongeza hatua ya maafikiano ya kumaliza mzozo wa Darfur baiana ya serikali ya Sudan na kundi la Justice and Equality movement JEM, yaliyotiwa saini mjini Doha Qatar.
Mpango wa usaidizi wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan UNAMA, hivi sasa unayapitia kwa undani maelezo ya mswaada wa sheria uliopendekezwa na Rais wa nchini hiyo Harmid Karzai ,ambao utampa mamlaka ya kudhibiti tume ya malalamiko ya uchaguzi.
Kundi la waasi lenye ushawishi mkubwa kwenye jimbo la Darfur na serikali ya Sudan wametia saini makubaliano ambayo yatafungua njia ya majadiliano ya kisiasa ili kumaliza miaka saba ya mvutano.
Mpango wa Umoja wa Mataifa unaohusika na Mazingira UNEP umesema nchi zote duniani lazima ziwe na hamasa ya ziada katika kupunguza kiwango cha gesi ya viwandani, endapo dunia inataka kweli kukabiliana na ongezeko la joto, na kulipunguza hadi nyuzi joto 2 au chini ya hapo.