Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na pale

Utafiti mpya wa Shirika la Afya Duniani (WHO) umegundua ya kuwa mama wajawazito, walioambukizwa na virusi vya UKIMWI wakipewa mchanganyiko wa madawa ya kurefusha maisha, kuanzia kile kipindi cha mwisho wa mimba hadi miezi sita ya kipindi cha kunyonyeshwa mtoto mchanga, asilimia 40 ya watoto wanaozaliwa na mama hawo hunusurika na hatari ya kuambukizwa na virusi vya maradhi. Jumuiya Mashirika ya UM dhidiya UKIMWI (UNAIDS) imeeleza na kukumbusha ya kwamba moja ya malengo muhimu ya kazi zao ni kuhakikisha wanafanikiwa kuzuia vifo vya mama wajawazito, na pia kuhakikisha watoto wachanga wanaozaliwa na mama hawo wanahifadhiwa na maambukizi ya VVU.

Hapa na Pale

Ashraf Qazi, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Sudan na Mkuu wa Shirika la Ulinzi Amani Sudan Kusini (UNMIS) ameripotiwa hii leo kuelekea eneo la mgogoro wa mpaka la Abyei, kwenye mkesha wa kutangazwa na Mahakama ya Upatanishi wa Abyei kutoka Hague maamuzi kuhusu eneo la mfarakano baina ya Sudan Kaskazini na Kusini. Uamuzi utatolewa na Mahakama ya Upatanishi Ijumatano. Mjumbe wa KM kwa Sudan Kusini alinakiliwa akisema hatua zimeshachukuliwa na wenye madaraka, za kuhakikisha makundi yote yenye silaha, isipokuwa Vikosi vya Pamoja vya Polisi na Jeshi, yameondoshwa kutoka Eneo la Mfarakano la Ramani ya Abyei kabla ya maamuzi kutangazwa kuzuia fujo.

FAO kuhadharisha Bonde la Mto Zambezi lasibiwa maradhi yanayouwa samaki

Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limehadharisha kwenye ripoti yake rasmi iliotolewa Ijumanne, ya kwamba kumegundulikana aina ya maradhi yenye kuua na kupunguza kwa kiwango kikubwa akiba ya samaki kwenye Bonde la Mto Zambezi, hali ambayo inahatarisha akiba ya chakula na ajira ya kujipatia rizki kwa wakazi wa vijijini wa eneo hilo, liliogawanyika miongoni mwa mataifa saba ya Afrika.