Mapigano Usomali kuwalazimisha maelfu ya raia kuhajiri Yemen kutafuta hifadhi
Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) kwenye taarifa iliyoiwasilisha Geneva, Ijumanne asubuhi, ilieleza mapigano yenye kuendelea hivi sasa kwenye mji wa Mogadishu, na katika eneo la kati la Usomali, yamesababisha maelfu ya raia kuhatarisha maisha kwa kuhama makwao, na kuamua kufanya safari hatari ya kuvuka Ghuba ya Aden, kuelekea Yemen kuomba hifadhi.