Mkutano wa UM kupinga ubaguzi waingia siku ya pili
Mkutano wa UM dhidi ya Ubaguzi wa Rangi Duniani unaofanyika mjini Geneva sasa hivi leo umeingia siku ya pili ambapo wawakilishi wa hadhi ya juu wamenedelea na mahojiano yao.
Mkutano wa UM dhidi ya Ubaguzi wa Rangi Duniani unaofanyika mjini Geneva sasa hivi leo umeingia siku ya pili ambapo wawakilishi wa hadhi ya juu wamenedelea na mahojiano yao.
KM Ban Ki-moon na Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu wameripotiwa kuchukuziwa na hotuba ya Raisi wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mahmoud Ahmadinejad aliowasilisha Ijumatatu kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Mapitio ya Mwito wa Durban na Mpango wa Utendaji wa Kupiga Vita Ubaguzi wa Rangi Duniani uliofanyika Geneva, Uswiss.
Mkutano wa UM juu ya Mapitio ya Mwito wa Durban dhidi ya Ubaguzi wa Rangi Duniani umeanza rasmi hii leo mjini Geneva. Kwenye risala ya ufunguzi, KM Ban Ki-moon alieleza masikitiko juu ya uamuzi wa baadhi ya nchi wanachama, wa kutohudhuria kikao hiki, licha ya kuwa ushahidi uliopo umethibitisha dhahiri kwamba ubaguzi wa rangi ni tatizo ambalo linaendelea kuselelea, na kujizatiti katika maeneo kadha wa kadha ya ulimwengu.
Kanayo Nwanzeon, Raisi wa Shirika la UM juu ya Mfuko wa Kimataifa kwa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) ameyasihi mataifa yenye maendeleo ya viwanda kuharakisha misaada yao maridhawa kwa wakulima wadogo wadogo, hasa wale waliopo katika nchi masikini, ruzuku ambayo anaamini ikitekelezwa kidharura itasaidia sana kwenye zile juhudi za kuuvua ulimwengu na mzoroto wa uchumi uliotanda kimataifa sasa hivi.
Shirika la UM juu ya Matumizi ya Amani ya Nishati ya Nyuklia (IAEA) limeandaa Mkutano wa Kimataifa mjini Beijing, Uchina uliokusanyisha mawaziri 30 wa nishati pamoja na wajumbe kutoka nchi 65, kwa madhumuni ya kuzingatia matumizi ya nishati ya nyuklia kwa karne ya ishirini na moja.
Navi Pillay, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu amepongeza maafikiano yaliokamilishwa, kwa mafanikio, na Kamati ya Matayarisho ya Mkutano wa Mapitio Kuhusu Mwito wa Durban dhidi ya Ubaguzi wa Rangi.
Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti, kwa kupitia msemaji wake mjini Geneva, kuwa na matumaini ya kutia moyo, kufuatia uamuzi uliochukuliwa wiki hii na serikali za Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK) na Rwanda, wa kukubali kuwasaidia raia waliohamia nchi mbili hiz kurudi makwao, kufuatia misiba kadha wa kadha iliolivamia eneo la Maziwa Makuu katika siku za nyuma.
Kutoka mji wa Oslo, Norway kumeanzishwa rasmi, leo Ijumaa, ushirikiano mpya wa kimataifa wa kuwasaidia mamilioni ya watu wanaogua maradhi ya malaria duniani, hasa wale wanaoishi katika nchi za Asia na mataifa ya Afrika kusini ya Sahara. Mradi huu utawapatia umma huo uwezo wa kumudu dawa za tiba ya malaria, dawa ambazo hunusuru maisha ya mgonjwa, hususan wale watoto wa umri mdogo.
Kwenye hotuba aliyoiwakilisha mbele ya wajumbe waliohudhuria warsha maalumu, leo asubuhi, katika Chuo Kikuu cha Princeton, kilichopo Jimbo la New Jersey, Marekani KM Ban Ki-moon alibainisha mtazamo wa sera mpya ya kimataifa juu ya uhusiano wa pande nyingi, miongoni mwa nchi wanachama.
Ahmedou Ould-Abdallah, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Usomali, amelaani vikali mashambulio ya karibuni yaliofanyika Mogadishu yaliowalenga wabunge, hujumu ambazo alisema zilikusudiwa hasa kuzorotisha juhudi za Serikali mpya ya Usomali za kupitisha Bungeni kanuni za Sharia, pamoja na kukwamisha zile jitihadi za kurudisha utulivu na amani ya eneo.