KM Ban Ki-moon ameripotiwa kushtushwa, kwa shambulio la kujitoa mhanga dhidi ya wachaMngu wa KiShia, liliotukia Ijumaa karibu na Baghdad. Kadhalika, KM alisema ameshtushwa na mashambulio mengine kama hayo yaliotukia majuzi Iraq ambayo yalisababisha darzeni za vifo na kujeruhi raia kadha wa kadha, ikijumlisha fungu kubwa la watoto wadogo na wanawake. KM alisisitiza hakuna sera ulimwenguni inayohalalisha vitendo hivi, si ya kidini wala kisiasa, na alikumbusha walimwengu wanawajibika, pote walipo, kulaani kwa lugha nzito kabisa makosa kama haya ya jinai kuu dhidi ya wanadamu. KM aliusihi umma wa Iraq kupinga kabisa jaribio katili linalotaka kuchochea fujo za kiitikadi nchini mwao, na aliwataka viongozi wa Iraq kuungana pamoja, kwa moyo wa kuhishimiana na uelewano wa kizalendo, kama walivyofanya wakati walipokwenda kupiga kura karibuni kwenye uchaguzi wa majimbo, uchaguzi ambao ulifanyika mwezi uliopita bila fujo.