Walimaji wadogo wadogo wa Tanzania wapatiwa mkopo na UM
Walimaji wa mashamba madogo madogo huko Tanzania watafaidika kutokana na mkopo wa dola milioni 56 unaopatiwa sekta ya kilimo ya serekali kutoka UM.
Walimaji wa mashamba madogo madogo huko Tanzania watafaidika kutokana na mkopo wa dola milioni 56 unaopatiwa sekta ya kilimo ya serekali kutoka UM.
Mkutano wa siku tatu kuhusu uchukuzi wa baharini, uliotayarishwa na Shirika la UM juu ya Biashara na Maendeleo (UNCTAD), umehitimisha mijadala wiki hii mjini Geneva kwa mwito uliohimiza wenye viwanda kuhakikisha wanaongeza juhudi zaidi kwenye ile kadhia ya kupunguza umwagaji wa hewa chafu angani.
Akiadhimisha kwa mara ya kwanza siku ya haki za kijamii duniani hii leo KM Ban Ki-Moon amesisitiza umuhimu wa kufuatilia haki za kijami kote duniani, akilalamika kwamba watu wengi kabisa hii leo wananyimwa haki hii, ambayo ni moja wapo ya msingi wa UM katika kazi zake za kuendeleza maendeleo na heshima kwa wote.
Hapa na Pale
Mji wa Copenhagen umesajiliwa Alkhamisi kuwa mshiriki wa 100 wa ushirikiano unaojulikana kwa umaarufu kama Mtandao wa Mazingira ya Hali ya Hewa Huru, ambao huongozwa na Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira (UNEP). Mwaka mmoja uliopita Mtandao wa Mazingira ya Hali ya Hewa Huru ulianzishwa rasmi kimataifa, kwa madhumuni halisi ya kukuza shughuli maalumu zitakazohakikisha umma wa kimataifa utaishi kwenye jamii zenye uchumi usiosumbuliwa na mazingira yaliopambwa na hewa chafu.
Ofisi ya msemaji wa KM imetangaza kwamba kuanzia wiki ijayo KM Ban Ki-moon atafanya ziara ya kuyatembelea mataifa matano barani Afrika, ikijumuisha Afrika Kusini, Tanzania, JKK, Rwanda na Misri.
Ijumaa ya tarehe 20 Februari itaadhimishwa rasmi, kwa mara ya kwanza na Shirika la UM juu ya Haki za Wafanyakazi (ILO) kuwa ni Siku ya Haki katika Jamii Duniani.
Ashraf Jehangir Khan, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Sudan, ambaye pia ni Mkuu wa Shirika la UM juu ya Amani Sudan Kusini (UNMIS) amenakiliwa, kwenye taarifa kwa waandishi habari, kusikitishwa sana na kifo cha mwandishi mashuhuri wa riwaya wa Sudan, Al-Tayeb Saleh kilichotukia wiki hii.
Jumuiya ya Mashirika ya UM Dhidi ya UKIMWI (UNAIDS) imekaribisha uamuzi wa Bunge la Burundi la kukataa ule mswada wa sheria ya kuharamisha usenge na ukhanithi nchini. Michel Sidibé, Mkurugenzi Mkuu wa UNAIDS amewasifu Wabunge kukataa marekibisho hayo, na anaamini kuwa wameonyesha ari kuu ya kutunza haki za binadamu za umma wao, kitendo ambacho anahisi ni cha kupigiwa mfano kwa wabunge wengine wa kimataifa. Kwa mujibu wa taarifa ya UNAIDS, uharamishaji wa tabia ya kijinsiya ya wanaume watu wazima na utenguzi wa haki za binadamu za watu wenye kuishi na virusi vya UKIMWI, ni mambo yenye kukwamisha juhudi za kudhibiti bora maambukizi ya VVU katika dunia, ambazo zinafungamana na fedheha ya uhalifu dhidi ya wasenge.