Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Baraza la Usalama kuridhia kuanzishwa ofisi ya kuimarisha amani Burundi

Baraza la Usalama limepitisha, kwa kauli moja, azimio la kuanzisha ofisi maalumu mpya nchini Burundi (Bureau Integre des Nations Unies au Burundi, BINUB)itakayopewa dhamana ya kusaidia kujenga utulivu wa kudumu nchini baada ya Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani (ONUB) kukamilisha operesheni zake mwisho wa mwaka (31 Disemba 2006).

Jukumu la wachoraji makatuni kustawisha amani duniani

Mapema wiki hii Idara ya Habari ya UM iliandaa semina maalumu iliyohudhuriwa na wachoraji makatuni mashuhuri wa kimataifa ambao walibadilishana mawazo juu ya taratibu zifaazo kutumiwa kwenye usanii wao zitakazosaidia kusukuma mbele amani na, hatimaye, kukomesha ile tabia ya kutovumiliana kati ya raia wa tamaduni tofauti. ~

Watu 126 wakhofiwa kufa kwenye Ghuba ya Aden

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR)limeripoti kwamba katika wiki za karibuni watu 126 kutoka Afrika Mashariki walifariki au kupotea walipokuwa wanajaribu kuvuka Ghuba ya Aden baada ya kutupwa majini kutoka meli na mashua za wafanya magendo.