Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wafanyakazi wa kimataifa washindwa kuhudumia raia muhitaji katika jimbo la Sudan la Darfur

Shirika la UM juu ya Operesheni za Amani katika Sudan, UNMIS, limeripoti karibuni ya kuwa wafanyakazi wa kimataifa wanaosimamia huduma za kiutu katika Darfur wanakabiliwa na vizingiti vinavyokwamisha huduma za kuwasaidia raia kupata mahitaji ya kunusuru maisha kwa sababu ya kuendelea kwa mashambulio na hali ya utumiaji nguvu dhidi yao, pamoja na vitendo vya uharamia na mapigano yalioshtadi kati ya makundi ya waasi.~~

Wanajeshi waangalizi wanne wa UM Kuuwawa Lebanon

Naibu KM wa Idara ya UM juu ya Operesheni za Amani Duniani, Jane Holl Lute aliripoti mbele ya Baraza la Usalama wiki hii kwamba wanajeshi waangalizi wanne wa ulinzi wa amani wasiochukua silaha kutoka Austria, Kanada, Finland ~na Uchina, waliuawa Ijumanne kwa mizinga ya majeshi ya Israel ambayo tuliarifiwa ililengwa moja kwa moja, sawia, kwenye kituo cha uangalizi cha UM karibu na mji wa Khiam, Lebanon ya kusini.

UM yaahidi kuongeza misaada ya kiutu Lebanon

Ilivyokuwa matatizo ya kiutu bado yanaendelea kukithiri katika mazingira ya vita katika Lebanon ya kusini UM umeripoti ya kuwa utalazimika kupeleka misafara ziada ya misaada ya kihali katika miji ya Jezzine na Sidon ili kukidhia mahitaji ya kunusuru maisha kwa umma waathiriwa wa maeneo haya. Hatua hii imechukuliwa baada ya msafara wa UM kufanikiwa Ijumanne kupeleka katika mji wa bandari wa Tyre shehena za chakula na mahitaji mengineyo ya kiutu.

Mwakilishi wa KM kwa Usomali apendekeza ujumbe wa kurudisha amani

Mwakilishi Maalumu wa KM kwa Usomali, Francois Lonseny Fall wiki hii amemtumia Sheikh Sharif Sheikh Ahmed, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Kundi la Mahakama za Kiislamu mjini Mogadishu barua inawayohimiza kupeleka wawakilishi wao kwenye duru ya pili ya mazungumzo ya kurudisha amani katika Somalia yaliyoandaliwa kufanyika Khartoum, Sudan kati yao na viongozi wa Serekali ya Mpito ya Usomali.

Hali ya mgogoro katika Mashariki ya Kati.

Alkhamisi KM Kofi Annan aliwakilisha mbele ya Baraza la Usalama, katika kikao cha hadhara, ripoti maalumu kuhusu hali katika Mashariki ya Kati, taarifa ambayo inaelezea matokeo ya juhudi za ujumbe wa maofisa watatu wa vyeo vya juu wa UM, waliozuru Mashariki ya Kati karibuni, kwa madhumuni ya kutafuta taratibu za kuridhisha kusitisha mapigano haraka na kuwasilisha suluhu inayokubalika na wote wahusika na mgogoro huo.~