Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Mtoto akiwa katika kambi ya wakimizi wa ndanijimboni Ituri nchini DRC  kufuatia kufurushwa makwao kutkana na mapigano mashariki mwa nchi
© UNICEF/Diana Zeyneb Alhindawi

Kikosi cha kwanza cha SADC chawasili DRC kusaidia kukabili mapigano mashariki mwa nchi

Huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wanajeshi wa kikosi cha kwanza kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika, SADC kitakachokuwa na jukumu la kusaidiana na jeshi la serikali, FARDC kujibu mashambulizi kutoka kwa vikundi vilivyojihami mashariki mwa nchi hiyo, wamewasili huko Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini.

Sauti
1'37"
Bukavu, Kivu Kusini. Uchaguzi wa Rais na wabunge umefanyika katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, 20 Desemba 2023.
MONUSCO/Michael Ali

DRC: Maisha yarejea hali ya kawaida huko Fataki, Ituri baada ya mashambulizi kutoka CODECO

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kazi ya kuhesabu kura inaendelea baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika Jumatano na kuendelea katika baadhi ya maeneo jana Alhamisi, huku ikielezwa kwamba jimboni Ituri, maisha  yamerejea katika hali ya kawaida kwenye eneo la Fataki baada ya mwaka mmoja wa mashambulizi kutoka kwa wanamgambo waliojihami wa kundi la CODECO. 

Sauti
1'20"
Uchaguzi wa rais na wabunge unafanyika katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
MONUSCO/Michael Ali

Uchaguzi mkuu DRC wafanyika kama ilivopangwa

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, uchaguzi mkuu wa Rais, Magavana, wabunge na madiwani umefanyika hii leo kama ilivyopangwa licha ya changamoto zilizojitokeza katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. Assumpta Massoi amefuatiliana na kutuandalia ripoti hii. 

Sauti
1'47"
Kampeni ya chanjo ya Polio nchini Tanzania.
UNICEF TANZANIA

Chanjo ya polio sio tu inamlinda mtoto bali inaokoa maisha: UNICEF

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linahimiza kila nchi kuhakikisha watoto wote wenye umri wa chini ya miaka 5 wanapatiwa chanjo dhidi ya polio ugonjwa ambao sio tu unasababisha ulemavu kwa watoto lakini pia ukakatili maisha yao. Kwa msaada kutoka wakfu wa Bill na Melinda gates hivi karibuni UNICEF na shirika la afya duniani WHO nchini Tanzania walizindua kampeni kubwa ya chanjo dhidi ya ugonjwa huo iliyowafikia watoto zaidi ya milioni 4.

Sauti
2'17"