Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Wanawake wakiwa wamejipanga mstari ili kupata chanjo dhidi ya Covid-19 nchini Malawi.
© UNICEF/ Thoko Chikondi

Ubunifu wa UNICEF Malawi kusambaza chanjo ya Covid-19 mtaa kwa mtaa wazaa matunda

Mnyumbuliko wa hivi karibuni wa virusi vya Corona vinavyosababisha Covid-19, Omicron ukiwa umesambaa ulimwenguni kote, ukosefu wa usawa wa chanjo unaweka baadhi ya watu hatarini zaidi kuruhusu minyumbuliko kubadilika na kuathiri wanadamu wengine. Afrika ina idadi ya chini zaidi ya watu waliochanjwa dhidi ya COVID-19 duniani lakini nchini Malawi mradi bunifu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF wa kusambaza chanjo kwa njia ya gari unaongeza upatikanaji wa chanjo na imani ya chanjo miongoni mwa wanawake wajawazito katika jamii za vijijini.

Sauti
1'57"
Mlinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, katika kikosi cha tano, TANBATT-5 kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa unaolinda amani nchini Mali, MINUSCA, akimsaidia mwanamke kubeba maji.
Meja Asia Hussein/TANBATT-5

TANBATT-5 wasambaza maji kwa wakazi wa Mambéré-Kadéï

Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANBATT-5 kwenye ujumbe wa umoja huo unaolinda amani nchini humo MINUSCA, kando mwa jukumu lao la ulinzi wa raia wamechukua jukumu la kusambaza huduma za maji safi na salama kwa wakazi wa maeneo  ambako wanalinda amani kama njia mojawapo ya kuimarisha ulinzi wa raia.

Sauti
1'32"
Wakulima wa mpunga wakichukua miche kwa ajili ya kupanda huko Nueva Vizcaya, Ufilipino.
© ILO/Joaquin Bobot Go

IFAD yasaidia wanawake wa kisiwani Sumar Ufilipino kujikomboa kiuchumi 

Mradi wa samaki unaofadhiliwa na Mfuko wa  Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo duniani FAO na Serikali ya Ufilipino, umekuwa mkombozi kwa wakina mama ambao hapo awali walikuwa hawana shughuli ya kuwaingizia kipato na sasa wanawake hao, wamejiinua kiuchumi kwa kutumia mbinu walizojifunza enzi za utotoni pamoja na utaalamu wa kisasa waliopatiwa.

Sauti
3'33"