Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Katibu Mkuu  António Guterres ametembelea maonesho ya picha ya "Mikononi mwao: Wanawake wachukua umiliko wa amani" katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa
UN Photo/Mark Garten)

Muda wa kurudisha nyuma saa ya haki za wanawake umepita, sasa iende mbele- Guterres alieleza Baraza

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu wanawake, amani na usalama ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wakati umefika kwa baraza hilo kuonesha kwa vitendo uungaji wake mkono wa harakati za wanawake katika ujenzi na uendelezaji wa amani badala ya kusalia maneno matupu.  Flora Nducha na maelezo zaidi.

Sauti
3'18"
Katika kituo cha ukusanyaji wa pamba Brazil ambako pamba hutenganishwa na mbegu kabla haijashindiliwa na kuhifadhiwa
FAO/Alberto Conti

Pamba, kitambaa kinachositiri  zaidi ya familia milioni 100 duniani:UN

 Leo ni siku ya pamba duniani ikiwa ni maadhimisho ya kwanza kabisa ya siku hiyo kuenzi zao ambalo kitabaa chake kinatengeneza mavazi ya kila siku yaliyosheheni kwenye mkabati mengi ya nguo na ni kitambaa kizuri, rahisi kuvaa, kukitunza na kinadumu kwa muda mrefu. Lakini kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa thamani ya pamba ni zaidi ya kitambaa kama inavyofafanua taarifa ya Flora Nducha 

Sauti
2'40"
Dr.Alinda Mashiku

Penye nia pana njia kama nimefika NASA nawe utaweza: Mhandisi Dkt.Alinda Mashiku 

Mwanamke Mtanzania angara kituo cha safari za anga cha Marekani NASA  tawi la Goddard mjini Maryland lililojikita na ufuatiliaji wa safari za satellite. Dkt. Alinda Mashiku ambaye amekuwa NASA kwa miaka minane sasa anasema ilimchukua miaka 12 hadi kuajiriwa NASA kama mhandisi na sasa pia ni meneja wa kitengo cha kuhakikisha satellite zonazokwenda angani hazigongani. Je anahisi vipi kuwa miongoni mwa wanawake wachache wahandisi NASA na safari yake ilianza vipi? Kufahamu yote hayo na mengine mengi ungana na Flora Nducha wa UN News Kiswahili aliyeketi na kuzungumza naye katika makala hii  

Sauti
13'39"
Utoaji wa chanjo dhidi ya COVID-19 nchini Kenya.
WHO Video

Kenya yaanza kutoa chanjo dhidi ya COVID-19 

Serikali ya Kenya inaendelea na kampeni ya chanjo dhidi ya corona au COVID-19 baada ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kupata na kusafirisha dozi zaidi ya milioni moja hadi Nairobi kupitia mkakati wa kimataifa wa upatikanaji wa chanjo COVAX. 

 

Sauti
2'43"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu MONUSCO nchini DRC wakizungumza na wananchi wakazi wa jimbo la Kivu Kaskazini.
TANZBATT_8/Kapteni Tumaini Bagambo.

TANZBATT_7 yafunga virago DRC na kukabidhi kijiti kwa TANZBATT_8

Kikosi cha 7 cha Tanzania, TANZBATT_7 kwenye kikosi maalum cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO kimetamatisha jukumu lake rasmi na kukabidhi bendera kwa kikosi cha 8 au TANZBATT_8. Shuhuda wetu kutoka Beni, jimboni Kivu Kaskazini ni Luteni Issa Mwakalambo, afisa habari wa TANZBATT_7. 

Sauti
3'19"