Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Bendera za Umoja wa Mataifa na ile ya Olimpiki zikiwa zinapepea kwa pamoja kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa
UN/Eskinder Debebe

COVID-19 yasababisha Olimpiki kusogezwa mwaka mmoja mbele, sasa kuchezwa 2021

Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki IOC na Kamati ya kimataifa ya Paralimpiki IPC au Olimpiki ya watu wenye ulemavu, kwa pamoja kamati ya maandalizi ya Tokyo 2020, Serikali ya mji wa Tokyo na serikali ya Japani wametangaza kuwa kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona, COVID-19, sasa michezo ya Olimpiki iliyokuwa ifanyike mwaka huu mjini Tokyo, itafanyika mwaka ujao wa 2021.

Sauti
3'24"
Kijana Tanzania atengeneza ndoo ya kunawa mikono bila kugusa koki wala sabuni.
UN News/ UNIC Tanzania

COVID-19: Kijana Tanzania atengeneza ndoo ya kunawa mikono bila kugusa koki wala sabuni

Ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 ukiwa umeshasambaa katika mataifa 199 ikiwemo Tanzania, vijana nao wanaibuka na ubunifu mbalimbali ili kusaidia mataifa yao katika kudhibiti kuenea kwa gonjwa hilo lisilo na tiba wala chanjo. Ubunifu wa vifaa vya kudhibiti kuenea umefanywa na kijana mmoja nchini Tanzania kama anavyoripoti… wa kituo cha habari za Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es salaam.

Sauti
2'