Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Kijana anayeishi Peru aliyepatikana kuwa anaishi na VVU mapema mwaka 2018
© UNICEF/Daniele Volpe

Kwa mwenendo wa sasa, takriban barubaru 76 watakufa kutokana na UKIMWI kila siku ifikapo 2030 -UNICEF

Vijana barubaru 76 wanakadiriwa kuwa watafariki dunia kila siku ulimwenguni kote kati ya mwaka hu una 2030 iwapo uwekezaji sahihi hautafanyika kuzuia Virusi Vya Ukimwi, VVU miongoni mwa kundi hilo, imesema ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF iliyotolewa leo kuelekea siku ya Ukimwi duniani tarehe mosi mwezi ujao.