Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mahojiano

Uganda yazindua kampeni ya chanjo dhidi ya kipindupindu-WHO

Kila mwaka nchini Uganda hutokea wastan wa visa1,850 vya kipindupindu na takriban vifo 45. Hii ni kwa mujibu wa waziri wa Afya wa Uganda Dkt Jane Ruth Acieng alipozungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo.

Visa vingi hutokea sehemu za Mashariki, Kaskazini na Kaskazini Magharibi mwa Uganda. Zoezi hili linadhaminiwa na  shirika la kimataifa la muungano wa chanjo ,GAVI na dawa inayotumika ya matone ndio inatumika kwa mara ya kwanza nchini Uganda.

Siraj Kalyango wa Idhaa hii amezungumza na waziri wa afya anehusika na shughuli za jumla , Dkt Sarah Opendi, kuhusu chanjo hii.

Sauti
2'41"

Utamu wa lugha ni pale inapotumiwa kwa ufasaha.

Kiswahili kimekuwa na mchango mkubwa kwa wazungumzaji wake hususan Afrika Mashariki kikipigwa jeki na vyombo vya habari kama Radio kwa miaka mingi. Lakini sasa hali ikoje katika kukuza na kuendeleza lugha hii?  Ken Walibora ni mwana riwaya na pia amekuwa mwandishi habari akitumia lugha ya Kiswahili miaka nena miaka rudi,  Katika mahojiano ,maalum na Siraj Kalyango wa Idhaa hii amezungumzia lugha hiyo na jinsi vyombo vya habari vinavyohusika kuiendeleza.

Sauti
3'19"