Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Prof. Chris Maina Peter na Tume ya kimataifa ya sheria ya UN

Bendera za mataifa wanachama wa UN193

Kwa ujumla tume imekuwa inasaidia Umoja wa Mataifa na jamii ya kimataifa katika kushughulikia sheria na hasa mikataba

UN Photo - Jean-Marc Ferre
Bendera za mataifa wanachama wa UN193

Prof. Chris Maina Peter na Tume ya kimataifa ya sheria ya UN

Masuala ya UM

Tume ya sheria ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa mwaka huu wa 2018 imetimiza  miaka 70 tangu iasisiwe. Tume hii Imefanya mengi katika kusongesha masuala ya kisheria. 

Tume ya sheria ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa mwaka huu wa 2018 imetimiza  miaka 70 tangu iasisiwe. Tume hii Imefanya mengi katika kusongesha masuala ya kisheria. Wajumbe wake ambao huchaguliwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa wanatoka nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania. Mjumbe huyo kutoka Tanzania ni Profesa Chris Maina Peter, Mhadhiri  wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam .Yeye akiwa  mjumbe wa tume hiyo hivi karibuni alihudhuria kikao mjini New York, Marekani na katika mahojiano maalum ma Siraj Kalyango wa Idhaa hii ameelezea mengi yaliyotekelezwa na tume ,lakini kwanza anaanza kwa  kueleza mafanikio ya tume hiyo hadi sasa.