Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Mama na mwanae wakiondoka kituo cha treni cha Lvivi nchini Ukraine.
© UNICEF/Giovanni Diffidenti

Mtu 1 kati ya 6 ni mkimbizi wa ndani Ukraine:IOM

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM inasema mtu 1 kati ya 6 ni mkimbizi wa ndani nchini  Ukraine na hivyo kuifanya idadi ya watu waliokimbia makazi yao na kusalia wakimbizi wa ndani tangu kuanza kwa mzozo wa Ukraine tarehe 24 mwezi Februari mwaka huu kufikia zaidi ya watu milioni 7.7 sawa na asilimia 17 ya watu wote wa taifa hilo.

Sauti
1'59"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António  Guterres akizungumza na wanahabari jijini New York, Marekani mbele ya bunduki iliyokunjwa inayoashiria usalama au bila mapigano.
UN /Eskinder Debebe

Pasaka ya waothodoksi Ukraine na Urusi ikikaribia, sitisheni mapigano kwa siku 4: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa siku nne za sitisho la mashambulizi nchini Ukraine kuanzia Alhamisi ya wikii hii wakati huu ambapo wiki takatifu ya kuelekea sikukuu ya PAsaka kwa waumini wa madhehebu ya kikristo ya kiothodoksi nchini Ukraine ikianza keshokutwa Alhamisi. Ametaka sitisho hilo liendelee hadi Jumapili tarehe 24 mwezi huu kilele cha Pasaka ya kiothodoksi.