Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashariki ya Kati

Palestina. Usambazaji wa mkate wa WFP katika shule ya UNRWA ambayo ni makazi maalum wakati wa dharura
© WFP/Ali Jadallah

Mfumo wa chakula Gaza umesambaratika kabisa: WFP

Mzozo unaoendelea Mashariki ya Kati umesambaratisha kabisa mfumo wa chakula Gaza limeonya shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP, likisisitiza wakati huu ambapo ni asilimia 10 tu ya bidhaa muhimu za chakula ndizo zinazoingia Gaza tangu kuanza kwa mzozo huo Oktoba 7. Hali ni mbaya na imesababisha njaa kwa karibu wate wote wa eneo hilo na tegemeo lao pekee lililobaki ni msaada wa chakula kutoka WFP.

Audio Duration
3'42"
Familia zinaendelea kupata hifadhi katika kambi ya Khan Younis huko Gaza.
© WHO

Israel yaonywa kutotumia maji na mafuta kama silaha za vita

Wakati mzozo wa Mashariki ya Kati ukiendelea na wananchi walioko Gaza wakiwa katika siku ya nne bila mawasiliano kutokana na ukosefu wa mafuta, mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki ya maji salama ya kunywa na usafi ameionya Israel kuwa kuwanyima wananchi maji ni ukiukaji wa haki za binadamu kwani wanatumia maji kama silaha ya vita. 

Sauti
2'58"
Maeneo makubwa ya Ukanda wa Gaza yameharibiwa na makombora.
© WHO

Madhila Gaza imetosha mambo 10 lazima yatekelezwe kuleta afueni: Griffiths

Umoja wa Mataifa leo umesisitiza kwa mara nyingine kwamba kinachoendelea Gaza ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu huku kukiwa na ripoti kwamba vikosi vya Israel vimevamia Hospitali ya Al-Shifa jana usiku ambako mbali ya wagonjwa kuna maelfu ya raia waliotawanywa wanapata hifadhi na umeonya kwamba hospital sio uwanja wa vita na madhila hayo kwa raia wakiwemo watoto lazima yakome kwa kutekeleza mambo 10 ya muhimu. 

Sauti
3'30"
(Maktaba) Mtoto akilia wakati mhudumu wa afya akimsogelea kutibu jeraha lake, Ni katika hospitali ya Al-Shifa mjini Gaza
UNICEF/Eyad El Baba

Maisha ya watoto yanaendelea kupotea Gaza huku hali ya kukata tamaa ikitawala: UN

Hali hatika hospitali za Gaza ni mbaya sana wagonjwa wakiendelea kupoteza maisha wakiwemo watoto njiti katika hospitali ya Al-Shifa ambayo kwa siku ya tatu mfululizo hakuna umeme huku mashambulizi ya Israel yakiongezeka, umesema Umoja wa Mataifa ambao leo unawaomboleza pia wafanyakazi wake 101 waliopoteza maisha katika mzozo huo na kusisitiza kwamba usitishwaji uhasama ni lazima sasa kuliko wakati mwingine wowote. 

Sauti
2'36"
Uharibifu mkubwa unaonekana katika ukanda wa Gaza kufuatia mashambulizi ya anga ya Israel tarehe 10 Oktoba 2023.
WHO

GAZA: Mashirika 18 ya Kimataifa yasema kwa kauli moja ‘imetosha’

Ikiwa ni siku 30 sasa tangu kuanza kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, kati ya Israel na Wanamgambo wa Kipalestina wa Hamas walioko katika eneo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu, Gaza, mashirika 18 ya Kimataifa ya misaada ya kibinadamu yametoa taarifa ya pamoja hii leo yakisema ‘imetosha’ wakitaka kusitishwa mara moja mzozo huo kwasababu za kibinadamu, mzozo ambao umegharimu maisha ya zaidi ya watu 10,000.

Sauti
4'12"
Mgonjwa anatibiwa katika Hospitali ya Nasser huko Khan Yunis kusini mwa Gaza.
© WHO

UN imekaribisha uhamishaji wa kwanza wa wagonjwa Gaza kwa ajili ya matibabu

Umoja wa Mataifa leo umekaribisha uamuzi wa Misri wa kukubali kupokea baadhi ya wagonjwa kutoka Gaza kwa ajili ya matibabu, huku mashirika mengine ya Umoja huo yakiendelea kuzungumzia adha inayowakabili maelfu ya watu wa Gaza wakiwemo watoto, uhaba wa mahitaji muhimu, ukosefu wa matuta, kufurika kwa makazi ya dharura na kuendelea kwa operesheni ya ardhini ya Israel.

Sauti
2'46"
Mashambulizi ya anga dhidi ya Gaza yanaendelea.
© WHO/Ahmed Zakot

Chonde chonde pande husika sitisheni huhasama, janga kubwa zaidi la kibinadamu laja Gaza: UN

Hali Mashariki ya Kati inazidi kuwa mbayá. Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo amezisihi pande zote katika mzozo kusitisha uhasama , huku mashirika ya misaada yakionya kuhusu janga kubwa zaidi la kibinadamu, wakati hapa Makao Makuu kikao cha 10 cha dharura kuhusu mzozo huo wa Mashariki ya Kati kikiendelea leo. 

 

Sauti
2'53"
Katibu Mkuu wa UN António Guterres akizungumza na wanahabari kwenye kivuko cha Rafah mpakani mwa Misri na Ukanda wa Gaza 20 Oktoba 2023
UN /Eskinder Debebe

Akiwa Rafah Katibu Mkuu wa UN asema shehena ya misaada inayosubiriwa ni mkombozi kwa walioko Gaza

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliyeko nchini Misri ametembelea mpaka wa Rafah ambacho ni Kivuko pekee cha kuingia na kutoka Ukanda wa Gaza, ambako hizo sasa kuna mashambulizi yanaendelea baina ya Israel na wanamgambo wa Hamas na kusema Umoja wa Mataifa hivi sasa unafanya mazungumzo ya kufafanua vikwazo na vizuizi vya masharti yaliyowekwa na Israel kabla ya kuruhusu misaada ya kibinadamu kuingia Ukanda wa Gaza.

Sauti
3'1"