Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Kambi ya wakimbizi ya Za'atari nchini Jordan inayoonekana kutoka juu ina wakimbizi kutoka Syria.
UN Photo/Mark Garten)

Watoto wangu wananiuliza Syria ni nini? Kambi ya Zaatar ikiingia muongo mwingine

Mwaka 2022 ni  miaka 10 tangu kuanzishwa kwa kambi ya wakimbizi ya Za’atari nchini Jordan, kambi ambayo inasimamiwa na Umoja wa Mataifa. Ni kambi kubwa zaidi Mashariki ya Kati na moja ya kambi kubwa zaidi duniani ikiwa ni maskani ya wasyria 80,000. UN News au Habari za UN imezungumza na baadhi ya wakimbizi kuhusu maisha katika kambi hiyo, na matumaini yao kwa siku zijazo. 

Mpaka wa Burundi na DR Congo. UNHCR inawasaidia wakimbizi wa Burundi waliokuwa DR Congo kurejea nyumbani.
Screenshot

Waliokuwa wakimbizi nchini DRC wafurahia kurejea nyumbani Burundi  

Raia 272 kutoka familia 78 wa Burundi waliorejea nchini Burundi kutoka kambi ya wakimbizi ya Lusenda katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwishoni mwa wiki iliyopita wamekaribishwa na wanachi wenzao, serikali na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi ili waanze maisha katika nchi yao waliyoikimbia kwa vipindi tofauti kutokana na hali mbaya ya usalama