Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Watoto wakimizi wakionesha kuunga kwao mkono shughuli za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR za kutokomeza usafirishaji haramu huko Wad Sharige Mashariki mwa Sudan.
© UNHCR/Osama Idriss

Simulizi Yangu: Kukabili usafirishaji haramu Malawi

Maxwell Matewere, mtaalamu katika ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuzuia uhalifu na madawa ya kulevya, (UNODC) nchini Malawi, amekuwa akiendelea na harakati zake za kukabiliana na usafirishaji haramu wa binadamu kwa zaidi ya miongo miwili. Leo hii anapatia mafunzo maafisa mbali mbali nchini Malawi kuzuia na kukabili uhalifu: mwaka huu pekee licha ya janga la Corona au COVID-19, ameweza kuokoa watu 300 waliokuwa wakumbwa na usafirishaji haramu sambamba na kukamata watu 31 wahusika wa uhalifu huo.