Shoroba za UN zitakuwa kimya,UNGA 75 itafanyika kupitia mtandao, mambo 5 ya kuyafahamu
Kikao cha 75 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA 75) kitaanza rasmi Septemba 15, na mwaka huu kutokana na janga la corona au COVID-19 linaloendelea mjadala utakuwa tofauti kabisa kuwahi kutokea katika historia ya chombo hicho kinachotimiza miaka 75 mwaka huu.