Uwekezaji katika elimu kwa watoto utawasaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi
Pazia la mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP28 likitarajiwa kufungwa hapo kesho huko Dubai Falme za kiarabu tunaangazia suala la jinsi mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri watoto hususani katika suala la Afya na kwenye elimu.
Tarehe 08 Desemba ratiba ya COP28 ilijikita mahususi kujadili masuala ya vijana na watoto. Mashirika mbalimbali yalitoa takwimu zinazohusiana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwa watoto na vijana moja wao ni Mfuko wa kimataifa wa elimu haiwezi kusubiri ECW.