Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

© UNICEF/Srishti Bhardwaj

UNITAID yahamasisha ufadhili wa Oksijeni

Kuelekea siku ya kimataifa ya kutokomeza ugonjwa wa Nimonia duniani, shirika la Umoja wa Mataifa la kufanikisha upatikanaji wa tiba nafuu UNITAID limetoa wito kwa washirika wote kuongeza kwa kasi ufadhili katika uzalishaji wa oksijeni na kujiunga na ubia wa kampeni ya  KILA PUMZI INAHESABIKA ili kuhamasisha kupunguza vifo vitokanavyo na uchafuzi wa hewa.

Leah Mushi anataarifa zaidi. 

Sauti
2'11"
FAO Tanzania

FAO imetufundisha kilimo cha wanyamakazi, nitapata kipato na kusaidia jamii- Kijana Gabriel

Mafunzo ya kilimo cha kutumia wanyamakazi yaleta nuru kwa vijana Kigoma (OVERNIGHT) 
Mafunzo yaliyoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo duniani, FAO  nchini Tanzania kwa vijana wakulima wilayani Kakonko mkoani Kigoma yameleta nuru ya kujiajiri na kujipatia kipato wakati huu ambapo Umoja wa Mataifa unataka vijana wasiachwe nyuma katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Taarifa ya Anold Kayanda inafafanua zaidi.  
 

Sauti
3'5"
IMF/K. M. Asad

Wakulima wabangladesh wateswa na mafuriko

Nchini Bangladesh mabadiliko ya tabianchi yamekuwa ni mwiba kwa maisha ya kila siku ya watu wa taifa hilo la Asia. Kwa mujibu wa mfuko wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo IFAD zaidi ya nusu ya watu milioni 90 wa nchi hiyo wanaishi katika maeneo yaliyoathirika vibaya na mabadiliko ya tabianchi huku wakikabiliwa na hatari kubwa ya mafuriko na wakulima ndio wanaobeba gharama kubwa ya zahma hiyo.

Sauti
2'36"
© UNICEF/Georges Harry Rouzier

UNESCO : Watoto walindwe na athari za mitandao ya kijamii

Kama nilivyokujulisha leo ni siku ya kimataifa ya kupinga uonevu na unyanyasaji shuleni na mtandaoni, shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO limeonya kwamba ingawa matumizi ya mtandao yanatoa fursa kubwa ya mawasiliano na kusoma pia yanawaweka watoto na vijana katika hatari kubwa ya ukatili na unyanyasaji.

Sauti
2'29"

Mauritania wapambana na mabadiliko ya tabianchi

siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano huo wa 26 wa nchi wanachama wa mabadiliko ya tabianchi, ambao hivi sasa unaendelea Glascow, Scotland, Mshauri Maalumu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudunia wakimbizi, UNHCR kuhusu Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi, Andrew Harper ametembelea Mauritania kujionea jinsi wakimbizi wanavyopambana na janga la tabianchi.

(Taarifa ya John Kibego)
“Hatujawahi kuona mwaka kama 2021. Huu ni mwaka wenye mioto mingi ya nyika.” Anasema Ahmedou El-Bokhary, Rais wa Kikosi cha zima moto kinachoundwa na wakimbizi.  

Sauti
2'5"
© WFP/Tsiory Andriantsoarana

Watu wote wa hapa kijijini tunakula majani ya madungusi kakati : Madagascar

Wakati mkutano wa mabadiliko ya tabianchi ungali ukiendelea huko Glasgow, Scotland, ukame unazidi kushika kasi kusini mwa Madagascar na watu wakiingia mwaka wa tano bila ya mvua hali inayowalazimu wananchi kula dungusi kakati kwa kuwa ndio mmea pekee unaoota kwenye maeneo yao.
(Taarifa ya Leah Mushi)

Mito! Ardhi Kame! Vumbi na watu wakisaka maji kwenye eneo kavu!

Ni taswira kutoka angani kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani WFP ya kijiji cha Marofanony kilichoko kusini mwa Madagascar!

Audio Duration
2'48"
State House Tanzania

Sasa tutoke kwenye maneno na ahadi, twende kwenye kufanya kweli kuhusu mabadiliko ya tabianchi: Rais Samia

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameelezea kile ambacho taifa lake na nchi nyingine zinazoendelea wanataka kuona kinatekelezwa baada ya mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP26 unaofanyika huko Glasgow Scotland.

Amesema hayo punde baada ya kuhutubia mjadala wa wazi wa mkutano huo unaofanyika wakati nchi tajiri zikisuasua kutekeleza ahadi zao akiongeza kuwa

Sauti
2'32"
UN Photo/Mark Garten)

Umoja wa Mataifa watoa wito kwa viongozi wa nchi kulinda waandishi wa habari

Pamoja na kufanya kazi kubwa ya kuhabarisha umma, waandishi wa habari ulimwenguni kote wanakabiliwa na mashambulio yanayohatarisha usalama wao ambapo mashambulio hayo ni pamoja na kauli za chuki, udhalilishaji kwenye mitandao ya kijamii, vurugu, ubakaji na hata mauaji. Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukomesha uhalifu dhidi ya waandishi wa habari Umoja wa Mataifa unasema muarobaini wa yote hayo ni utashi wa kisiasa.